Saturday, October 19

Ahukumiwa kwenda chuo cha mafunzo.

 

Kijana  Khamis  Shaib Khatib  mwenye umri wa miaka  24 mkaazi  wa Kizimbani Wete Pemba ahukumiwa kwenda  chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka  saba  [7]  na kutozwa faini ya shilingi laki mbili za kitanzania baada   ya  kupatikana na hatia ya kumbaka  msichana wa miaka kumi na tatu [13].

Hukumu hiyo imesomwa na  hakimu  Abdala  Yahya  Shamuhun  baada  ya kuona ushahidi uliotolewa mahakamani hapo unaridhisha.

Hakimu huyo alimtaka mshitakiwa huyo kwenda kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka  saba [7] na kutozwa fidia ya shilingi laki mbili baada ya mahakama kumtia hatiani kwa kosa la kubaka.

“Mtuhumiwa umepatikana na hatia kwa  kosa la  kubaka  utatumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka  saba[7]” alisema shamuhun.

Kabla ya kusomewa shitaka lake hilo mshitakiwa alipewa nafasi ya kujitetea ambapo aliomba mahakama impunguzie adhabu, ombi hilo lilipingwa na upande wa mashtaka.

“Muheshimiwa hakimu naomba munipunguzie adhabu kwani sitorudia tena kosa hili” alieleza mshitakiwa huyo.

Mwendesha mashtaka kutoka  ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka [dpp]  ali amour makame aliomba mahakama kumpa adhabu kali mshitakiwa huyo ambapo hilo litakua ni funzo kwa wengine.

Ilidaiwa mahakamani hapo  siku isiofahamika mwezi 11/2019 majira ya sa 3;  kamili za asubuh huko Kizimbani Wilaya ya Wete Pemba ulimbaka msichana wa miaka 13, kufanya kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 108 [1], [2], [e] na 109 [1] sheria nambari 6/2018, sheria ya Zanzibar.