Sunday, March 16

VIDEO: Watendaji wa TASAF Kisiwani Pemba watakiwa kuhakikisha walengwa wanatambuliwa kwa usahihi.

 

NA SHEKHA SEIF

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh. Salama Mbarouk Khatib amewaagiza watendaji wa mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF Kisiwani Pemba kuhakikisha walengwa wanatambuliwa kwa usahihi ili kuondoa uwezekano wa kuwa   na walengwa wasiokidhi vigezo.

Muheshimiwa Salama amesema hayo huko katika ukumbi wa Jamhuri  Wete  katika kikao cha kujenga uelewa kuhusu kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya mpango huo,  kilichowashirikisha wadau wa TASAF Mkoa wa kaskazini Pemba.

Amesema mfuko huo umekuja na mpango wa kuzinusuru kaya masikini hivyo ni vyema kwa wasimamizi hao kufuata miko na maelekezo yanayotakiwa ili adhima ya serikali iweze kufikiwa huku akisisitiza kwamba Serikali haitosita kuwachukulia hatua watakao kwenda kinyume na agizo hilo.

Kwa upande wake mtendaji wa Tasaf Makao Makuu ndugu Makaza Manyagula Makaza amesema utekelezaji wa Mpango wa kunusuru  kaya masikini umewezesha kujikita katika kukuza uchumi wa walengwa.

Naye Mratib wa TASAF Pemba ndugu Mussa Said amesema zoezi la utambuzi wa kaya masikini lina changamoto nyingi hivyo ni vyema kwa watendaji hao kua makini  katika  kuziainisha na kushirikiana kwa pamoja pale panapohitaji  kuzipatia ufumbuzi.

ANGALIA VIDEO HAPA CHINI