Thursday, September 19

Bonanza la Michezo kwa taasisi za Serekali lazinduliwa kisiwani Pemba.

YOTE HII NI KASI YA DR. MWINYI ,BONANZA LA MICHEZO LINAWEZEKANA.

Na Maryam Taalib – -Pemba.

MKUU wa Wilaya ya Chake Chake  Abdalla Rashid  amewataka watendaji wa Taasisi pamoja na wananchi kwa ujumla kujenga utamaduni wa  kuimarisha afya zao kupitia michezo tofauti  ili kuondokana na kupata maradhi hatarishi.

Ameyasema hayo wakati akizindua Bonanza  la michezo  katika uwanja wa Gombani Kongwe Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba ikiwa ni katika heka  heka za kusherehekea kwa kutimiza miaka (60) ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Alisema  amefarajika kwa kiasi kikubwa kuona wanataasisi wamejitokeza kwa wingi katika mashindo hayo ya michezo tofauti tofauti.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya alimpongeza  Ofisa  Mdhamini Wizra ya Habari Vijana Utamaduni  na Michezo Pemba Mfamau Lali Mfamau  kwa kuwa mbunifu mzuri wa kuzinsha Bonanza  hilo  ikiwemo michezo ya wanawake.

“Nawaombeni  wana taasisi na wananchi kwa ujumba huu ni mwanzo mzuri ambao tunaenda nao  tunatakiwa tuwe tunacheza hii michezo kila baada ya muda na sio tusubirie kila ifikapo kusherehekea sherehe za Mapinduzi kama tulivojizowesha.”alisema Rashid

Kwa upande wake Afisa mdhamini Wizara ya habari Vijana Utamaduni na Michezo Mfamau  Lali Mfamau  alisema  Mapinduzi yamekuja kumkomboa mwananchi  na hii inaonekana  kwa anaefahamu tulipotoka ,tulipo na tunakoelekea,  haya yote   na mengineo ni hatua kubwa ya maendeleo katika nchi yetu.

Mfamau alisema  amefurahishwa sana kwa kuona ushiriki mkubwa  wa wanawake  kwa kushiriki na kushindana katika michezo tofauti katika Bonanza hilo la  kusherehekea kuelekea  miaka (60) ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Mchezaji  mwanamke kutoka Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo  Nd, Hamisa Omar Hamad aliweza kunyakua ushindi wa kufukuza kuku pamoja na ushindani wa kukuna nazi katika Bonanza hilo.

“Kwa kweli michezo  tunahitaji kuiendeleza mara kwa mara kama Mdhamini alivyotuanzishia kwenye washindani wengi ushindi ni jambo zito leo tumejinyakulia Wizara ya habari mashindani ”alisema Hamisa.

Tasisi Kumi na moja   za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kisiwani Pemba ambazo zimeingia katika mashindano hayo ya kusherekea Miaka (60) ya Mapinduzi Matukufu  ya Zanzibar.

MWISHO.