Saturday, March 15

ELIMU

Walimu na wanafunzi washauriwa kuvitumia vituo vya HUB kujiendeleza kielimu.
ELIMU

Walimu na wanafunzi washauriwa kuvitumia vituo vya HUB kujiendeleza kielimu.

  NA SAID ABRAHMAN.   WALIMU na Wanafunzi Kisiwani Pemba, wametakiwa kuvitumia vituo vya HUB ili waweze kujiendeleza kitaaluma.   Kauli hiyo imetolewa na Ofisa Miradi kutoka taasisi ya Milele Zanzibar Foundation Fatma Hamad, wakati akifungua mafunzo ya ELIMIKA yaliyoandaliwa na taasisi hiyo, kwa walimu wa Pemba huko katika kituo Cha HUB Kilichopo Skuli ya Sekondari Limbani Wete.   Alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha walimu kuweza kupata ujuzi wa kutumia mitandao, ili kuweza kuwafundisha wanafunzi kutumia njia ya mtandao katika masomo yao na  kuwawezesha kufanya vizuri katika mitihani yao.   Aidha alifahamisha kuwa hivi Sasa mambo yamebadilika, hivyo aliwasisitiza walimu hao kuwashajihisha wanafunzi wao kutumia zaidi mitandao ...
ELIMU

Uboreshwaji wa masomo ya hesabati, sayansi na kiengereza utasaidia kuimarisha mfumo wa elimu kwa wanafunzi.

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA NAIBU Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Korea (KOICA) Jieun Seong amesema, uboreshwaji wa masomo ya hesabati, sayansi na kiengereza utasaidia kuimarisha mfumo mzima wa elimu kwa wanafunzi. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo kazini yaliyofanyika katika Ukumbi wa Benjamin Wete Mkoa wa Kaskazini, Naibu huyo alisema kuwa, jukwaa hilo la viongozi watakaopewa mafunzo wanaamini litachangia katika kutekeleza maendeleo ya elimu nchini. Alisema, elimu ni ufunguo wa maisha, hivyo wanataka kuboresha elimu katika masomo ya hesabati, sayansi na kiengereza kwa kuweka mazingira bora ya ufundishaji, kutoa vifaa pamoja na kuwaongezea uwelewa walimu na wanafunzi. "Tunawaomba mutoe mapendekezo hapa na tunaahidi tutayafanyia kazi kwa ajili ya kujenga...
Mwalimu mwenye ulemavu wa viungo aomba msaada wa kujengewa madrasa yake
ELIMU, Kitaifa

Mwalimu mwenye ulemavu wa viungo aomba msaada wa kujengewa madrasa yake

NA FATMA HAMAD. Mwalimu wa madrasa Juhudiya ,Sada Khamis Hamad ( mwenye ulemavu wa Viungo) ilioko Shumba Vyamboni Wilaya  ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba  amesema anakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa sehemu salama ya kusomeshea Wanafunzi  kutokana na hali yake. Akizungumza na mwandishi wa habari  hizi huko nyumbani kwao mwalimu huo alisema mazingira ya madrasa yake sio rafiki, kwani anatumia kibaraza cha nyumba yao kuwafundishia Wanafunzi wake. ‘’Nasumbuka sana  hususan kipindi cha mvua barazani panakua hapasomeki inabidi wanafunzi  wasije madarasa mpaka mvua zikate.’’alisema mwalimu bi Sada. Sada alieleza kuwa mwanzo alikua akienda madrasa  maeneo ya mbali kwa ajili ya kusoma lakini badae  akashindwa  kutokana na hali yake, kwani alikua hawezi kut...
Jamii yatakiwa kushirikiana ili kukomesha vitendo vya udhalilishaji.
ELIMU, Kitaifa

Jamii yatakiwa kushirikiana ili kukomesha vitendo vya udhalilishaji.

NA ABDI SULEIMAN.   JAMII imeshauriwa kushirikiana kwa pamoja katika kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia wa wananwake na watoto, ili jamii iendelee kuishi katika hali ya amani.   Alisema iwapo jamii itakubali kusimama kidete na kuunda mikakati ambayo itaweza kufanikisha kutokomezwa kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia watoto wataishi kwa amani na utulivu.   Ushauri huo umetolewa na Afisa Utetezi na Mawasiliano kutoka taasisi ya NCA Tanzania Nizar Selemani Utango, kwenye mkutano wa msafara wa vijana wa kuhamasisha amani na mtengamano wa jamii, kupitia utekelezaji wa mradi wa mtengamano wa jamii na amani Zanzibar unaotekelezwa na taasisi za kidini, huko Tumbe Wilaya ya Micheweni.   Alisema suala la amani na utulivu ni jambo la uhimu s...