Saturday, March 15

ELIMU

Walimu wa skuli za msingi kisiwani Pemba watakiwa kuwa na utayari wa kuyatumia mafunzo ya Jifunze kwa hatua.
ELIMU

Walimu wa skuli za msingi kisiwani Pemba watakiwa kuwa na utayari wa kuyatumia mafunzo ya Jifunze kwa hatua.

NA SAID ABRAHMAN.   MRATIBU wa Skuli za Sekondari Kisiwani Pemba Suleiman Hamad Suleiman, amewataka walimu wanaoshiriki mafunzo ya "Jifunze kwa hatua" kuwa na utayari ili wawe chachu kwa walimu wengine.   Alisema kuwa endapo walimu hao wataweza kuyafuatilia kwa umakini mafunzo hayo, watakuwa ni kigezo kikubwa kwa walimu wenzao ambao wako nyuma na kuwafanya nao waende na wakati.   Hayo aliyaeleza kwa niaba ya Ofisa Mdhamini wa Wizara ya elimu na mafunzo ya amali Pemba, Mohammed Nassor Salim, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya"Jifunze kwa hatua"(TaRL), yaliyoandaliwa na taasisi ya Milele Foundation huko katika kituo Cha science Pujini Wilaya ya Chake Chake Pemba.   Mratibu huyo alisema kuwa chanzo Cha baadhi ya wanafunzi kutoweza kusoma, kuandika pamo...
Ufunguzi wa Kongamano la Nane Zanzibar la Kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
DINI, ELIMU, Kitaifa

Ufunguzi wa Kongamano la Nane Zanzibar la Kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haitamvumilia yoyote atakaejihusisha na matendo ya udhalilishaji kwa lengo la kumaliza kabisa tatizo hilo. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dkt Hussein Ali Mwinyi ametoa kauli hiyo katika Hotuba iliyosomwa kwa Niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla wakati akizindua Kongamano la Nane la kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan lililofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar. Amesema Serikali imejipanga na inaendelea kuchukua hatua kali dhidi ya wanaojihusisha na matendo hayo ambayo yanaiathiri jamii hasa kwa vizazi vijavyo. Alhajj Dkt Mwinyi amesema imefika hatua kwa wananchi kuacha muhali na kutowaonea huruma wafanyaji wa vitendo hivyo ili kuisaidia Se...
Sanaa yarindima Wete.
ELIMU, Utamaduni, vijana

Sanaa yarindima Wete.

(PICHA NA SAID ABDULRAHMAN PEMBA)   NA SAID ABRAHAMAN. MASHINDANO ya elimu bila malipo Wilaya ya Wete Kwa Kanda ya Mashariki yameendelea tena mwishoni juma lililopita kwa upande wa sanaa, kwa skuli za msingi na sekondari.   Michezo ambayo ilifanyika hapo ni pamoja na sanaa ya ushauri, utenzi, wimbo, ngonjera pamoja na tamthilia ambapo Skuli hizo ziliweza kutoa burudani mwanana kwa watazamaji waliofika katika viwanja hivyo.   Katika sanaa ya ushauri, mshindi kwa upande wa msingi iliweza kuchukuliwa na Skuli ya Minungwini ambayo ilijipatia alama 175 sawa na asilimia 87.5%, nafasi ya pili ikinyakuliwa na Mjini Kiuyu kwa kupata alama 155 sawa na asilimia 77.5% huku mshindi wa tatu ikiwa ni Skuli ya Jojo ambayo ilijipatia alama 151 sawa na asilimia 75.5%....