Saturday, March 15

ELIMU

Waziri SMZ wawafariji wanafunzi Skuli ya Utaani .
ELIMU

Waziri SMZ wawafariji wanafunzi Skuli ya Utaani .

NA ABDI SULEIMAN. SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka wazazi, wanafunzi na walimu wa skuli ya Utaani Sekondari, kuwa wastahamilivu na wavumilivu, na kufahamu kuwa mtihani uliotokea ni mipango ya Mwenyezi Mungu imeshaandikwa. Imesema kutokea kwa mtihani wa kuungua kwa modo weni la wanafunzi wanawake, haitokua sababu ya kurudi nyuma kimasomo badala yake masomo yataendelea siku zote hususana kwa wanafunzi ambao wanajindaa na mitihani yao ya kidatoi cha sita. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Lela Mohamed Mussa, alipokua akizungumza na wazazi, walimu na wanafunzi huko skuli ya Utaani, kwa lengo la kuwafariji waathirika wa tukio hilo. Alisema suala la elimu ni jambo muhimu sana kwa watoto, aliwataka wanafunzi kuzidisha juhudi katika m...
KAMISHENI YA ARDHI YAKUTANA NA MASHEHA WIYALA YA WETE
ELIMU, Kitaifa

KAMISHENI YA ARDHI YAKUTANA NA MASHEHA WIYALA YA WETE

NA ABDI SULEIMA. MASHEHA Wilaya ya Weye Mkoa wa Kaskazini Pemba, wamewashauri wananchi kfuata sheria na taratibu wakati wanapotaka kuuziana ardhi au kurithishana, ili kupunguza migogoro isiyo kuwa ya lazima. Wamesema kuwa kumekua kukijitokeza migogoro mingi ya ardhi katika jamii, unapofuatilia inatokana na sheria kupindishwa wakati wa mauziano au urithishaji wake. Masheha waliyaeleza hayo wakati walipokua wakizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kumalika kwa kikao cha kujadili masuala ya ardhi na utatauzi wa migogoro, huko Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba. Sheha wa shehia ya Kipangani Makame Seif Faki, alisema licha ya elimu kutolewa kwa jamii, bado migogoro ya ardhi imekua ikijitokeza kidogo kidogo, kufuatia sheria kutokufuatwa wakati wa kuuziana kwa mali. “K...
TAASISI za Ifraji Zanzibar Foundation na  Milele Zanzibar Foundation zawafariji wanafunzi Utaani.
ELIMU, Kitaifa

TAASISI za Ifraji Zanzibar Foundation na Milele Zanzibar Foundation zawafariji wanafunzi Utaani.

  NA ABDI SULEIMAN. TAASISI ya Ifraji Zanzibar Foundation na Milele Zanzibar Foundation, zimekabidhi vifaa mbali mbali kwa wanafunzi wa skuli ya Sekondari Utaani vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 40. Wanafunzi hao ambao bweni lao la kulalia lilipata mtihani wa kuungua moto wiki iliyopita, huku vitu vyao mbali mbali vikiteketea katika tukio hilo. Akizungumza katika hafla ya kupokea msaada huo kwa wanafunzi 64 wa kidato cha sita kwa hatua ya kwanza, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Lela Mohamed Mussa, alizishukuru taasisi hizo kwa kuwajali wanafunzi hao pamoja na kuguswa na tukio hilo. Alisema taasisi hizo zimekuwa za kwanza kuwasaidia wanafunzi hao baada ya tukio lililotokea, kwani msaada huoumefika katika kipindi muwafaka ikizingatiwa mwaka huu wana...
Waziri Mkuya: Waandishi ibueni changamoto za watu wenye ulemavu.
ELIMU, Kitaifa

Waziri Mkuya: Waandishi ibueni changamoto za watu wenye ulemavu.

NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Saada Mkuya Salim amewataka waandishi wa habari visiwani Zanzibar kuibua changamoto zinazowakwaza watu wenye ulemavu ili kuiwezesha Serikali kuziona, jambo ambalo litasaidia kupatiwa ufumbuzi wa haraka. Alisema kuwa, watu wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ambazo zinahitaji kutatuliwa, hivyo ni jukumu la waandishi kuziibua na kuzitangaza ili nao wapate haki zao zinazostahiki. Aliyasema hayo wakati akifungua mkutano wa siku mbili kwa waandishi wa habari katika Ukumbi wa Hoteli ya Maru Maru mjini Unguja. "Kila mmoja kwa nafasi yake ana jukumu la kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapatiwa haki zao na nyinyi waandishi ni sauti ya wasio na sauti, hivyo tujitahidi kuwasemea wenzetu hawa",...
TMDA KUTOA TUZO KWA WAANDISHI WA HABARI ZINAZOHUSU UDHIBITI WA DAWA, VIFAA TIBA NA BIDHAA ZA TUMBAKU
afya, Biashara, ELIMU, Kitaifa

TMDA KUTOA TUZO KWA WAANDISHI WA HABARI ZINAZOHUSU UDHIBITI WA DAWA, VIFAA TIBA NA BIDHAA ZA TUMBAKU

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), imeandaa tuzo maalumu kwa kazi za Waandishi wa Habari juu ya Udhibiti wa Dawa, Vifaa tiba, Vitenganishi na bidhaa za tumbaku kwa mwaka 2021-2022. Kwa mujibu wa taarifa ya TMDA, tuzo hizo ni kwa Waandishi wa Habari ambao wameripoti taarifa na kuandaa makala mbalimbali kuhusu kazi na majukumu ya TMDA katika kipindi cha kuanzia Juni 2021hadi Februari mwaka huu. “Lengo ya tuzo hizo ni kutambua mchango wa Waandishi wa Habari na kuleta hamasa katika kuelimisha jamii kuhusu masuala ya udhibiti wa dawa, vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa za tumbaku kupitia vyombo vya habari ili kulinda afya za jamii.” Ilieleza taarifa hiyo ya TMDA Aidha, imebainisha kuwa, kazi zinazolengwa ni zile zilizoripotiwa kupitia Televisheni (TV), Redio, Magazeti na mit...