Saturday, March 15

ELIMU

VYOMBO VYA HABARI VISAIDIE DUNIA KUPUNGUZA HOFU ZITOKANAZO NA HABARI POTOFU KWENYE MAPIGANO YA URUSI NA UKRAINE
ELIMU, Kitaifa

VYOMBO VYA HABARI VISAIDIE DUNIA KUPUNGUZA HOFU ZITOKANAZO NA HABARI POTOFU KWENYE MAPIGANO YA URUSI NA UKRAINE

Na Gaspary Charles. Naiona hatari kubwa sana mbeleni ya athari za kisaikolojia ulimwenguni (world psychological effects by fake news) kutokana na kushamiri na kusambaa  kwa kasi sana taarifa potofu juu ya mapigano yanayoendelea kati ya Urusi na Ukraine. Licha ya mzozo huu kufikia hatua mbaya sana, lakini ni wazi kwamba taarifa zisizo sahihi juu ya kinachoendekea Ukraine mpaka wakati huu ndizo zimechukua nafasi kubwa masikioni mwa watu hasa kupitia mitandao ya kijamii jambo linalozidisha  wasiwasi zaidi na taharuki kuwa kubwa zaidi duniani kuliko uhalisia wa jambo lenyewe lilivyo. Kwa siku mbili mtawalia nimefuatilia kwa ukaribu vyanzo mbalimbali vya habari kutoka 'viwanja vya mapigano' na ni ukweli usiopingika kwamba hali kwasasa ni mbaya kwa maeneo hayo lakini zip...
Wanafunzi 412 wapatiwa elimu juu ya kuepuka migogoro na udhalilishaji.
ELIMU

Wanafunzi 412 wapatiwa elimu juu ya kuepuka migogoro na udhalilishaji.

NA ABDI SULEIMAN. JUMLA ya wanafunzi 412 kutoa skuli sita katika Wilaya ya Wete na Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, wamefikiwa na Jumuiya ya Kuwezesha Vipaji vya Vijana Pemba (YETA), kwa ajili ya kupatiwa elimu juu ya kuepuka migogoro na udhalilishaji katika kipindi cha uchumaji wa zao la Karafuu. Wanafunzi hao waliopatiwa elimu na Jumuiya hiyo ni kutoka skuli za Sekondari Kinyasini, IstiQaama, Mgogoni, Konde, Mabatini na Gando. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, Msaidizi afisa mradi wa kujenga uelewa kwa vijana, katika kuzuia migogoro ya ukatili kipindi cha mavuno ya zao la karafuu Pemba, Omar Abrahman Suleiman, alisema YETA imeona kipindi cha uchumaji wa karafuu matukio mengi hujitokeza kwa jamii ndio wakaamua kutoa elimu hiyo maskulini. Alis...
Wanafunzi 17124 wameanza masomo yao ya awali  Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa mwaka 2022.
ELIMU

Wanafunzi 17124 wameanza masomo yao ya awali Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa mwaka 2022.

NA ZUHURA JUMA, PEMBA KIASI Cha wanafunzi 17124 wameanza masomo yao ya awali katika Skuli mbali mbali za Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa mwaka 2022.   Kwa upande wa Skuli za maandalizi wanafunzi walioandikishwa ni 4623, walioanza darasa la Kwanza ni 10,090 na Wanafunzi wanaosoma tutu ni 2411.   Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake, Ofisa elimu Mkoa wa Kaskazini Pemba Khamis Said Hamad alieleza kuwa wanafunzi hao ni wale ambao muda wao wa kuanza  kusoma umefika.   Alifahamisha kuwa kwa upande wa Wilaya ya Wete wanafunzi ambao walioandikishwa ni 7,797 ikiwa maandalizi ni wanafunzi 2538 na kwa darasa la awali (darasa la Kwanza) 5259.   "Wilaya ya Wete wanafunzi ambao wameandikishwa ni 7,797 ikiwa wavulana ni 4081 na wasichan...
RAIS WA ZANZIBAR ALHAJ DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEJUMUIKA KATIKA SALA YA IJUMAA NA WANANCHI WA KIJITOUPELE NA KUMJULIA HALI BWANAKHERI OMAR NYUMBANI KWAKE KIEMBESAMAKI
ELIMU, Kitaifa

RAIS WA ZANZIBAR ALHAJ DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEJUMUIKA KATIKA SALA YA IJUMAA NA WANANCHI WA KIJITOUPELE NA KUMJULIA HALI BWANAKHERI OMAR NYUMBANI KWAKE KIEMBESAMAKI

  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasailimia Waumini wa Dini ya Kiislam baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Qudus Kijitoupele Wilaya ya Magharibi “A” Unguja.    WAUMINI wa Dini ya Kiislam wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj.Dk.Hussein Ali Mwinyi.(hayupo pichani) wakati akizungumza na kuwasalimia Wananchi baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Qudus Kijitoupele Wilaya ya Magharibi “A” Unguja RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Mahmoud Mussa Wadi, baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masj...
SMZ INATAMBUA UMUHIMU WA WATAALAM WA TEHAMA NCHINI
ELIMU, Kitaifa

SMZ INATAMBUA UMUHIMU WA WATAALAM WA TEHAMA NCHINI

SERIKALI ya Mapinduzi  Zanzibar inatambua umuhimu ya kuwa na wataalam wa TEHAMA wabobezi wenye ujuzi mahiri kwa maslahi ya maendeleo ya Taifa.  Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Mhe. Rahma Kassim Ali alieleza hayo katika hafla ya ufunguzi wa Semina ya wataalamu wa TEHAMA iliofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar. Mhe. Rahma amesema Serikali zote mbili zimewekeza kwa kiasi kikubwa katika kutoa elimu ya TEHAMA kulikowezesha kuzalisha wataalamu ambao kutokana na mabadiliko ya kasi wanahitaji kuwendelezwa ili kukabiliana na changamoto za maendeleo ya TEHAMA. Alieleza kuwa, Mbali na kuendeleza wataalamu wa TEHAMA, SMZ kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi imekuwa ikitoa  ushirikiano wa kutosha katika kukuza ubunifu na tafiti m...