PPC yapongezwa kuhamasiaha Amani katika jamii
NA ABDI SULEIMAN.
WANANCHI wa Shehia ya Wawi Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, wameipongeza Jumuiya ya waandishi wa habari Pemba (PPC),kwa maamuzi yao ya kuelimisha jamii juu ya suala zima la utunzaji wa Amani iliyopo nchini.
Wamesema ni jumuiya chache zenye moyo wa kufanya jambo kubwa kama hilo, kupita katika shehia mbali mbali na kuhamasisha jamii juu ya suala zima la utunzaji wa amani.
Kauli hiyo imetolewa na sheha wa shehia hiyo, Sharifa Waziri Abdalla, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wazi juu ya kuelimisha jamii kuhusu masuala ya Amani, Umoja na Mshikamano, kupitia mradi wa SAUTI YANGU, AMANI YANGU, HATMA YANGU, naotekelezwa na PPC wakishirikiana na Foundation for civil society na Search for common groud, kwa ufadhili wa umoja wa nchi za ulaya.
Sheha sharifa ali...