WANAWAKE Pemba wataja changamoto wanzokumbana nazo kufikia uongozi ndani ya siku 16 za kupinga udhalilishaji.
NA ABDI SULEIMAN
WAKATI Mataifa mbali mbali yakiungana Duniani, katika siku 16 za kupiga ukatili wa kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto, Tanzania ni miongioni mwa nchi zinaendelea na kampeni hiyo kila mwaka.
Niwazi bado matukio ya udhalilishaji, yamekua ni changamoto kubwa katika jamii hali inayopelekea kukata tama kwa wanaharakati.
Siku hii ilianzishwa mwaka 1991 ikiongozwa na kituo cha kimataifa cha wanawake, Zanzibar nayo inaungana na watanzania katika kuadhimisha siku hiyo, ikiwemo makongamano, mikutano, warsha za vijana, wanafunzi na midahalo ya watoto na watu wazima.
Makala haya imeangalia changamoto au vikwazo wanavyokumbana navyo wanawake, wanapoingia katika masuala ya uongozi katika nafasi mbali mbali.
Changamoto hizo ni pamoja na Rushwa, imani potofu kw...