Friday, March 14

ELIMU

WANAWAKE Pemba wataja changamoto wanzokumbana nazo kufikia uongozi ndani ya siku 16 za kupinga udhalilishaji.
ELIMU, Makala, Sheria, Wanawake & Watoto

WANAWAKE Pemba wataja changamoto wanzokumbana nazo kufikia uongozi ndani ya siku 16 za kupinga udhalilishaji.

  NA ABDI SULEIMAN WAKATI Mataifa mbali mbali yakiungana Duniani, katika siku 16 za kupiga ukatili wa kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto, Tanzania ni miongioni mwa nchi zinaendelea na kampeni hiyo kila mwaka. Niwazi bado matukio ya udhalilishaji, yamekua ni changamoto kubwa katika jamii hali inayopelekea kukata tama kwa wanaharakati. Siku hii ilianzishwa mwaka 1991 ikiongozwa na kituo cha kimataifa cha wanawake, Zanzibar nayo inaungana na watanzania katika kuadhimisha siku hiyo, ikiwemo makongamano, mikutano, warsha za vijana, wanafunzi na midahalo ya watoto na watu wazima. Makala haya imeangalia changamoto au vikwazo wanavyokumbana navyo wanawake, wanapoingia katika masuala ya uongozi katika nafasi mbali mbali. Changamoto hizo ni pamoja na Rushwa, imani potofu kw...
Citizen Brigade kisiwani Pemba wametakiwa kuendelea kufuatilia na kuibua changamoto zinazowakwaza wanawake.
ELIMU, Kitaifa

Citizen Brigade kisiwani Pemba wametakiwa kuendelea kufuatilia na kuibua changamoto zinazowakwaza wanawake.

Na Gaspary Charles- TAMWA ZNZ MKURUGENZI wa Chama cha waandishi wa habari Wanawake Tanzania, TAMWA- Zanzibar Dkt. Mzuri Issa Ali, amewataka wahamasishaji jamii kwa wanawake kudai haki zao za uongozi na demokrasiua kisiwani Pemba kuendelea kufuatilia na kuibua changamoto zinazowakwaza wanawake kukosa haki zao katika nyanja mbalimbali kwenye jamii Mkurugenzi huyo ametoa kauli hiyo wakati wa mkutano baina ya watendaji wa TAMWA ZNZ, PEGAO na wahamasishaji hao wenye lengo la kujadili na kutathimini maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo kisiwani humo unaofadhiliwa na Ubalozi wa Norway. Alisema lengo la mradi kuwatumia wahamasishaji hao ni kutaka wafanye kazi ya kukutana na wanajamii kwa lengo la kubaini changamoto zinazowakabili na kuwasaidia uwezo wa kudai haki zao katika masuala mbalimb...
WALIMU wa madrasa za Qur-ani waishauri serikali kumfungia mwalimu atakaebainika kujihusisha  na vitendo vya udhalilishaji.
ELIMU, Sheria

WALIMU wa madrasa za Qur-ani waishauri serikali kumfungia mwalimu atakaebainika kujihusisha na vitendo vya udhalilishaji.

\ NA HANIFA SALIM, PEMBA WALIMU wa madrasa za Qur-ani Kisiwani Pemba wameishauri serikali endapo itambaini mwalimu wa madrasa kujihusisha na matendo ya udhalilishaji kumfungia na badala yake kumchukulia hatua kali ili kukomesha ambao wana tabia kama hizo. Walisema, kuna baadhi ya walimu wa madrasa wamekua wakijihusisha na matendo ya udhalilishaji kwa wanafunzi wao jambo ambalo linawapotezea heshima walimu hao ndani ya jamii zao. Waliyasema hayo wakitoa michango katika mafunzo hivi karibuni yaliyoandaliwa na ofisi ya mufti kupitia ofisi Rais katiba, sheria, utumishi wa umma na utawala bora yaliyofanyika ukumbi wa ofisi ya Rais fedha na mipango Gombani Chake chake. Mjumbe wa jumuiya ya maendeleo Wilaya ya Wete Abubakar Hassan Suleiman, aliipongeza ofisi ya mufti ya kuwapatia...
Uwandani wanataka elimu ya kisheria.
ELIMU, Sheria

Uwandani wanataka elimu ya kisheria.

NA ABDI SULEIMAN. WANANCHI wa Uwandani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba, wamesema kuwa bado elimu ya kisheria haijawafikia na wanahitaji kupatiwa elimu hiyo ili waweze kujuwa wapi wafuate haki zao za kisheria pale wanapozikosa. Walisema wamekuwa wakikosa haki zao mbali mbali muda mrefu sasa, hivyo watakapopatiwa elimu hiyo wajuwa wapi wafikishe malalamiko yao ili kudai haki zao. Waliyaeleza hayo katika mkutano wa wazi ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, katika siku 16 za kupoga vita vitendo vya udhalilishaji wa wanawake na watoto nchini. Salum Juma Hamadi mkaazi wa Uwandani, alisema masuala ya udhalilishaji uwandani yapo na yameshakuwa mzingo, huku wananchi wakishidwa kujuwa wapi pakupata haki zao baada ya kukosa elimu. “Tumekuwa...
afya, ELIMU

Vyoo 12 vyajengwa skuli ya Ole, sasa wanafunzi waondokana na kujisaidia vichakani

NA ABDI SULEIMAN. LICHA kupata msaada wa kujengewa Matundu 12 ya Vyoo na Mdau wa Maendeleo, lakini bado matundu hayo hayajakidhi mahitaji ya wanafunzi wa skuli ya Ole Msingi Wilaya ya Chake Chake katika suala la vyoo. Skuli hiyo yenye wanafunzi 1849, inahitaji angalau matundu ya vyoo 50, ambalo tundu moja litaweza kutumiwa na wanafunzi 37 kwa wakati mmoja. Matundu hayo yameweza kujengwa na mdau huyo, kufuatia taarifa iliyoatolewa na Gazeti la Zanzibar leo Toleo NO:6335 la Septemba 8/2021 ukurasa wa tano inayosema skuli ya kosa vyoo wanafunzi wajisaidia vichakani, msiktini na toleo NO:6425 Novemba 16/2021 ukurasa wa 12 na 13 inayosema Uhaba wa vyoo waikabili skuli ya ole Msingi. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, kufuatia ujenzi huo wa matundu 12 ya vyoo Mwalimu Mku...