Thursday, March 13

ELIMU

MUFTI mkuu afungua msikiti na kuwataka waislamu kuendeleza amani
ELIMU, Kitaifa

MUFTI mkuu afungua msikiti na kuwataka waislamu kuendeleza amani

  NA ABDI SULEIMAN, MUFTI Mkuu wa Zanzibar Shekh Saleh Omar Kaabi, amewataka wananchi wa sompiya kuwa na moyo wa kushirikiana, katika kutatua matatizo ya jamii zao na maeneo ya jirani, ili amani na utulivuo iendelea kudumua. Mfufti Mkuu aliyaeleza hayo wakati alipokua akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu na wananchi wa shehi ya Sompiya, mara baada ya kufungua mskiti kijijini hapo. Shekh Kaabi alisema pahala patakatifu katika ardhi ni mskitini, kwani mskiti usipotumiwa kwa kusali utawasuta, hivyo unapaswa kutumiwa kufanya ibada na kuwahimiza watoto kusali. “Tunapaswa kuutumia msiki kwa mambo mema, ikiwemo kuweka darsa mbali mbali, kuwasomesha watoto wetu mambo mema, tutumie pia kusuluhishana migogoro inayotoka katika jamii”alisema. Naye katibu wa Muft Shekh Kh...
RAIS MHE.DKT. MWINYI AHUDHURIA MAHAFALI YA 40 YA CHUO KIKUU HURIA TANZANIA YALIOFANYIKA UWANJA WA NMAO ZEDUNG
ELIMU

RAIS MHE.DKT. MWINYI AHUDHURIA MAHAFALI YA 40 YA CHUO KIKUU HURIA TANZANIA YALIOFANYIKA UWANJA WA NMAO ZEDUNG

MKUU wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Mhe Mizengo Peter Pinda akimtunuku Shahada ya Udaktari wa Falsafa mhitimu Bakari Ali Mohammed,  wakati wa mahafali ya 40 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania yaliofanyika katika Uwanja wa Mao Zedung Jijini Zanzibar Wilaya ya Mjini Unguja leo 25-11-2021.(Picha na Ikulu)  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia katika hafla ya Mahafali ya 40 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania yaliofanyika katika Uwanja wa Mao Zedung Jijini Zanzibar leo 25-11-2021, na (kushoto kwa Rais) Prof.Deus Ngaruko Naibu Makamu Mkuu wa Chuo (Taaluma) na Prof.Elifas Bisanda Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania.(Picha na Ikulu) na Ikulu) MKUU wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Mhe.Mizengo Peter Pinda akiwatunuku Shahada ya Uzamivu ya Udaktari w...
Benki ya Dunia yaunga mkono hatua ya serikali ya Tanzania kuwarejesha wasichana shuleni
ELIMU

Benki ya Dunia yaunga mkono hatua ya serikali ya Tanzania kuwarejesha wasichana shuleni

Benki ya Dunia imeunga mkono tangazo la Serikali ya Tanzania la kuondoa vikwazo vya upatikanaji wa elimu, vikiwemo vile ambavyo vimewazuia wasichana wajawazito au kina mama wachanga kuhudhuria shule katika mfumo rasmi. Uamuzi huu muhimu unasisitiza dhamira ya nchi ya kusaidia wasichana na wanawake vijana na kuboresha nafasi zao za kupata elimu bora, ilisema taarifa ya benki hiyo. Benki ya dunia imesema zaidi ya wasichana 120,000 huacha shule kila mwaka nchini Tanzania. 6,500 kati yao kwa sababu ni wajawazito au wana watoto. ''Benki ya Dunia inaunga mkono kwa dhati sera zinazohimiza elimu ya wasichana na zinazowezesha wanafunzi wote kusalia shuleni. ''Benki inatarajia kutoa miongozo itakayowawezesha wasichana wajawazito na kina mama vijana kuendelea na masomo...
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said Azungumza na Ujumbe wa Chuo Kikuu cha Potsdam cha Ujerumani.
ELIMU

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said Azungumza na Ujumbe wa Chuo Kikuu cha Potsdam cha Ujerumani.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Simai Mohammed Said akimkabidhi kitabu cha Historia ya Tanzania, Rais wa Chuo Kikuu cha Potsdam cha Ujerumani Profesa Oliver Gunther, baada ya kumaliza mazunumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Elimu Mazizini Jijini Zanzibar. Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said amesema Wizara itaendeleza mashirikiano na Wadau mvalimbali wa Elimu ili kuhakikisha maendeleo yanapatikana katika Sekta hiyo. Mhe  Simai ameyasema hayo wakati alipokuwa na mkutano na ujumbe kutoka Chuo Kikuu cha Potsdam nchini Ujerumani, katika Ukumbi wa Wizara hiyo Mazizini Mjini Unguja. Ameushukuru ujumbe huo kwa kuja Zanzibar kujenga mashirikiano ambapo amesema kuna haja ya kujengewa uwezo walimu wao ili nao waweze kut...