Wednesday, March 12

ELIMU

afya, ELIMU, Kitaifa

VIDEO: DC Mkoani alishukuruku shirika la UNESCO kwa kuiunga mkono Wilaya hio.

NA  KHADIJA KOMBO-PEMBA Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja amelishukuru shirika la Kimataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni  (UNESCO) kwa juhudi zake za kuiunga mkono Wilaya hio kwa miradi mbali mbali ya maendeleo ndani ya jamii. Mkuu huyo wa Wilaya ametoa pongezi hizo huko ofisini kwake wakati alipokutana na Mkurugenzi Mkaazi na Mwakilishi wa  UNESCO nchini Tanzania aliyefika Ofisini kwake huko Mkoani mara baada ya uzinduzi wa kituo cha Makuzi na malezi ya watoto huko Skuli ya Msingi Mkanyageni katika Wilaya ya Mkoani. Amesema Serikali ya Wilaya inathamini juhudi za Shirika hilo na kuahidi kufanya kazi nao kwa pamoja ili kuinua ustawi wa jamii hasa watoto katika upatikanaji wa elimu. Kwa Upande wake Mkurugenzi Mkaazi na mwakilishi wa  UNESCO nchini Tanzania Bwana Tirso...
ZRB yawataka wananchi kudai risiti
Biashara, ELIMU, Kitaifa

ZRB yawataka wananchi kudai risiti

  BODI ya mapato zanzibar ZRB imewataka wananchiu kudai risiti baada ya kufanya matumizi yao,  kwani ni uthibitisho wa kutosha kuwa mali ulionayo ni yako au unaimiliki kihalali. bodi hiyo imesema unapodai risiti unaisaidia serikali kupa kiwango cha Kodi kinachostahiki kutokana na mauzo hayo. aidha imesema risiti inakupunguzia usumbufu kutoka katika vyombo vya dola kama vile Polisi na  Mahakamani inapotokea haja ya kufanya upekuzi kwa mali ambayo imeibiwa.
IFRAJI yakabidhi jengo la skuli ya maziwa Ng’ombe Micheweni
ELIMU, Kitaifa

IFRAJI yakabidhi jengo la skuli ya maziwa Ng’ombe Micheweni

NA ABDI SULEIMAN. KUKABIDHIWA kwa banda moja lenye madarasa mawili ya kusomea wanafunzi wa skuli ya Msingi Mwiza Ngombe Wilaya ya Micheweni, kutoka kwa Taasisi ya Ifraji Zanzibar Foundation, itapelekea kupunguza msongamano wa wanafunzi kutoka 85 hadi 65 kwa darasa moja. Hayo yameelezwa na Mwalimu Mkuu wa Skuli hiyo Kombo Rashid Hilali, wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhiwa kwa banda moja lenye vyumba viwili vya kusomea lililogharimu Milioni 27. Alisema licha ya skuli hiyo kuingia mikondo miwili asubuni na mchana, lakini wanafunzi darasani hukaa 85 hali inayopelekea kuwa ngumu kwa mwalimu wakati wa kufundisha na kupitia wanafunzi mmoja mmoja. “Skuli yetu tuna madarasa 12 na wanafunzi 2118 wanaume ni 952 na wanawake 1169, lakini haipe...