Saturday, March 15

Kimataifa

Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 01.07.2021: Sancho, Rice, Kane, Sterling, Haaland, Mbappe
Kimataifa, Michezo

Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 01.07.2021: Sancho, Rice, Kane, Sterling, Haaland, Mbappe

Huku makubaliano ya kumsaini winga wa Borussia Dortmund Jadon Sancho yakiafikiwa , kiungo wa kati wa West Ham Declan Rice ,22, beki wa Villareal mwenye umri wa miaka 24 Pau Torres na mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane 27 , ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na mkufunzi wa Man United Ole Gunnar Solskjaer (Guardian) Sancho atapatiwa jezi nambari saba katika klabu ya Manchester United ambayo kwa sasa inavaliwa na mshambuliaji wa Uruguay Edinson Cavani, 34. (Metro) United pia ina hamu ya kumsajili kiungo wa kati wa Bayern Munich Leon Goretzka, 26, ambaye kandarasi yake na klabu hiyo ya Bundesliga inakamilika 2022.. (Bild - in German) CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES Maelezo ya picha,kiungo wa kati wa Bayern Munich Leon Goretzka ...
Haya ni mataifa matano ambayo mwanamke anaweza kuolewa na wanaume zaidi na mmoja
Kimataifa

Haya ni mataifa matano ambayo mwanamke anaweza kuolewa na wanaume zaidi na mmoja

Umewahi kufikiria kuwa na mume mwenza katika ndoa? Swali hili ni kwa wanaume, lakini kwa wanawake umewahi kufikiria kuolewana wanaume wawili? Au Unakumbuka tukio la mkazi mmoja wa Makueni huko Kenya, Rael Mukeku, aliyeamua kuolewa na wanaume wawili lilivyosambaa kwenye vyombo vya habari? Ama tukio la Maurine Atieno kutoka eneo la Migori nchini humo alivyotiwa nguvuni baada ya kukiri kuolewa na wanaume wawili? Ni kawaida hasa kwa jamii ambazo imani ya kiislamu imetawala, kuona mwanaume akiwa na mke zaidi ya mmoja, lakini si jambo la kawaida hasa kwa jamii nyingi kuona wanaume wawili wakimuoa na kuishi na mwanamke mmoja. Yapo mataifa duniani ambayo ndoa ya mwanamke mmoja kuolewa na wanaume wawili ni kitu cha kawaida kabisa kupitia mila za makabila yao na kuwekewa utaratibu ...
AirCar: Gari linalopaa angani lafanikiwa kuruka kutoka uwanja mmoja wa ndege hadi mwengine
Kimataifa

AirCar: Gari linalopaa angani lafanikiwa kuruka kutoka uwanja mmoja wa ndege hadi mwengine

Gari la mfano linaloweza kupaa angani limekamilisha dakika 35 angani kati ya viwanja vya ndege huko Nitra, na Bratislava nchini Slovakia. Gari hilo kwa jina 'Aircar'{Gari ndege} lina injini ya gari la BMW na hutumia mafuta ya petroli. Muundaji wake Profesa Stefan Klein , anasema kwamba linaweza kupaa angani kwa zaidi ya kilomita 1000 na urefu wa juu wa futi 8,200 na kufikia sasa limefanikiwa kukaa angani kwa saa 40. Inachukua dakika mbili na sekunde 15 kubadilika kutoka kuwa gari hadi ndege. 'linapendeza' Mbawa zake nyembamba hujikunja kando kando ya gari hilo. Profesa Klein aliiendesha katika barabara ya ndege hadi mjini alipowasili , akitazamwa na waandishi wa habari walioalikwa. Alielezea uzoefu huo mapema siku ya Jumatatu kama wa kawai...
Waziri wa afya wa Uingereza Matt Hancock aomba msamaha baada ya picha yake ‘akimbusu’ msaidizi wake kuvuja
Kimataifa

Waziri wa afya wa Uingereza Matt Hancock aomba msamaha baada ya picha yake ‘akimbusu’ msaidizi wake kuvuja

Waziri wa Afya wa Uingereza Matt Hancock amekiri kuvunja masharti ya kutokaribiana baada ya kupigwa picha akimbusu mmoja wa wasaidizi na picha hiyo kuchapishwa kwenye gazeti moja. Alisema kwamba "amewaangusha watu" baada ya kuonekana kwenye picha akiwa na Gina Coladangelo - aliyemteua - na kuomba "msamaha". Chama cha Labour kimemuomba Waziri Mkuu kumchukulia hatua Bwana Hancock, kikitaja nafasi aliyopewa kuwa amepewa mtu"asiyefaa". Lakini Bwana Boris Johnson amesema kwamba ameukubali msamaha wa Bwana Hancock na "kuchukulia kuwa suala hilo limeisha". Waziri Mkuu aliulizwa kama "ana imani" na Bwana Hancock, msemaji wa Waziri Mkuu alijibu: "Ndio." Gazeti la The Sun limeripoti kuwa picha za Bwana Hancock na Bi Coladangelo, ambao wote kila mmoja ...
Tetesi za Soka Ulaya Ijumaa 25.06.2021: White, Malen, Grealish, Xhaka, Braithwaite, McGinn, Saliba
Kimataifa, Michezo

Tetesi za Soka Ulaya Ijumaa 25.06.2021: White, Malen, Grealish, Xhaka, Braithwaite, McGinn, Saliba

Maelezo ya picha,Kiungo wao wa kati wa Aston Villa Jack Grealish Aston Villa wanaamini watasalia na kiungo wao wa kati Jack Grealish,25, ambaye ananyatiwa na Manchester City, Chelsea na Manchester United. (Athletic, subscription required) Wawakilishi wa Grealish, hata hivyo wanapendekeza aondoke Villa, katika hatua ambayo itamwezesha kupata paUni milioni 100 akiahamia Manchester City. (Sun) Arsenal wamepiga hatua katika mazungumzo yao na Brighton kuhusu mkataba wa mlinzi wa Uingereza Ben White, 23, ambao huenda ukawa wa thamani ya zaidi ya pauni milioni 50. (Sky Sports) CHANZO CHA PICHA,BBC SPORT Maelezo ya picha,Arsenal wamepiga hatua katika usajili wa mlinzi wa Brighton, Ben White Klabu hiyo ya ...