Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 01.07.2021: Sancho, Rice, Kane, Sterling, Haaland, Mbappe
Huku makubaliano ya kumsaini winga wa Borussia Dortmund Jadon Sancho yakiafikiwa , kiungo wa kati wa West Ham Declan Rice ,22, beki wa Villareal mwenye umri wa miaka 24 Pau Torres na mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane 27 , ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na mkufunzi wa Man United Ole Gunnar Solskjaer (Guardian)
Sancho atapatiwa jezi nambari saba katika klabu ya Manchester United ambayo kwa sasa inavaliwa na mshambuliaji wa Uruguay Edinson Cavani, 34. (Metro)
United pia ina hamu ya kumsajili kiungo wa kati wa Bayern Munich Leon Goretzka, 26, ambaye kandarasi yake na klabu hiyo ya Bundesliga inakamilika 2022.. (Bild - in German)
CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,kiungo wa kati wa Bayern Munich Leon Goretzka
...