Saturday, March 15

Kimataifa

Waridi wa BBC: Mfahamu Mkuu wa Wilaya ya Temeke Tanzania Jokate Mwegelo
Kimataifa

Waridi wa BBC: Mfahamu Mkuu wa Wilaya ya Temeke Tanzania Jokate Mwegelo

Anne Ngugi BBC Swahili Maelezo ya picha,Mkuu wa Wilaya ya Temeke nchini Tanzania Jokate Mwegelo Jokate Mwegelo ni mwanamke mwenye umri wa miaka 34 na licha ya umri wake mdogo ni mkuu wa Wilaya ya Temeke , iliyopo Dar es Salaam Tanzania. Mbali na hilo pia ni mmoja ya wanawake waliofanikiwa katika medani ya urembo nchini humo baada ya kuchukua nafasi ya pili katika mashindano ya malkia wa urembo nchini Tanzania mwaka 2006. Anapoulizwa kuhusu swala la urembo yeye hutabasamu tu, akionesha mwanya uliopo kati ya meno yake, hali kadhalika kidoti cheusi kinachoshirikishwa na urembo kilichopo usoni mwake. Sio vigumu kwa mtu anayemtafuta mkuu huyu wa wilaya miongoni mwa umati kumkosa kutokana na muonekano . Vilevile bi Joketo ni miongoni mwa vijana maa...
Oparesheni Barbarossa: Maswali 10 ya kuelewa ‘kosa baya zaidi’ la Hitler katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia
Kimataifa

Oparesheni Barbarossa: Maswali 10 ya kuelewa ‘kosa baya zaidi’ la Hitler katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia

Maelezo ya picha,Propaganda ilikuwa kiungo muhimu katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia. Wasovieti kama inavyoonekana katika picha hii , walijaribu kuweka ari juu katika kupinga uvamizi wa Nazi Mnamo Juni 22, 1941, Wanazi wa Ujerumani walizindua oparesheni Barbarossa, dhidi ya Muungano wa Soviet ambayo wakati huo ilikuwa ikiongozwa na José Stalin. Ulikuwa uvamizi mkubwa wa kijeshi katika historia, na dau hatari ambalo Adolf Hitler alitumia kubadili hatma ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia kwa maslahi yake. Lakini mambo hayakuenda kama alivyopanga, na wanahistoria wanachukulia kufeli kwa oparesheni hiyo kuwa mwanzao wa na mwisho wa nguvu ya Ujerumani. Operasheni Barbarossa ilikuwa mwanzo wa miezi sita ya vita vikali kati ya madola mawili ya kiimla, ambayo ...
Mchungaji Bushiri: ‘Mhubiri anayeweza kutembea angani’
Kimataifa

Mchungaji Bushiri: ‘Mhubiri anayeweza kutembea angani’

Watu wanapiga makofi, wengine wanacheza densi na wengine wakirukaruka juu huku akiingia katika ukumbi , akiandamana na walinzi wake. Hiyo ndio furaha ambapo baadhi ya waumini ambao walikuwa wamemsubiri kwa saa tano kumuona wanazirai. Lakini kwanini wewe usizirai? Huyu ni mtu ambaye anasema kwamba ametibu watu wenye virusi vya HIV, amewafanya vipofu kuona, amebadilisha hali ya masikini na mara moja ameonekana akitembea angani. Mtumishi wa Mungu kwa jina Bushiri amepitia mengi akilewa katika mji wa Mzuzu uliopo kaskazini mwa Malawi. Siku hizi , anaweza kujaza viwanja vya michezo na maelfu ya waumini wake ni wafuasi ambao wako tayari kusafiri kote duniani ili kumuona akiongoza ibada yeye mwenyewe. CHANZO CHA PICHA,KANISA LA ECG Ana w...
Fahamu ukweli kuhusu kikosi cha wanawake pekee kilichokuwa kikimlinda Muammar Gaddafi
Kimataifa

Fahamu ukweli kuhusu kikosi cha wanawake pekee kilichokuwa kikimlinda Muammar Gaddafi

Tangu kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Libaya Muammar Gaddafi mikononi mwa kundi la waasi mnamo Oktoba 2011 mengi yameandikwa na kusemwa juu yake. Lakini hakuna mengi yaliyosemwa kuhusu , kikosi cha walinzi wa kike ambao walikuwa akiandamana naye kote katika safari zake . Alijulikana kwa kuwapenda wanawake na kiongozi huyo wa zamani wa Libya alioa mara mbili. Alikuwa na wake wawili, binti na mamia ya walinzi wa kike waliokuwa wakijihami vikali kwa bunduki.Kulikuwa pia na muuguzi wa Kiukreni na wafuasi wengi wanawake ambao walisimama karibu naye wakati wa maisha yake. Mkewe wa kwanza, alikuwa mwalimu wa shule. Walitengana baada ya miezi sita na wana mtoto wa kiume - Muhammad. Mkewe wa pili, Safia al-Gaddafi, muuguzi kwa taaluma, ndiye mama wa wanawe wengine saba. ...
Ilikuaje kwa mwanajeshi wa zamani kukatwa uume wake na mkewe?
Kimataifa

Ilikuaje kwa mwanajeshi wa zamani kukatwa uume wake na mkewe?

Mnamo tarehe 23 Juni 1993 mke mchanga alikata uume wa mumewe katika shambulio lililowashangaza wnegu . Mke huyo alikuwa Lorena Bobbitt - na mume wake alikuwa John Wayne Bobbitt - na kisa hicho kilizungumzia kote duniani . Kwa wale wanaokumbuka, kisa hicho ,kumbukumbu hizo bado zipo na siku kama hii ya leo ambapo ulimwengu unaadhimisha siku kupambana na dhulma za kijinsia. Kisa cha Lorena Bobbit na mume wake John kinaleta vyema taswira ya jinsi dhulma katika ndoa au uhusiano zinavyoweza kugeuka na kuwa kitu kibaya zaidi au hata maafa . Miaka ishirini na nane iliyopita, huko Manassas, Va., Mwanamke mwenye umri wa miaka 24 alikata uume wa mumewe na kisu cha jikoni. Jina lake lilikuwa Lorena Bobbitt. Kilichofuta na habari za tkio hilo kugonga vichwa vya habari nchini M...