Waridi wa BBC: Mfahamu Mkuu wa Wilaya ya Temeke Tanzania Jokate Mwegelo
Anne Ngugi BBC Swahili
Maelezo ya picha,Mkuu wa Wilaya ya Temeke nchini Tanzania Jokate Mwegelo
Jokate Mwegelo ni mwanamke mwenye umri wa miaka 34 na licha ya umri wake mdogo ni mkuu wa Wilaya ya Temeke , iliyopo Dar es Salaam Tanzania.
Mbali na hilo pia ni mmoja ya wanawake waliofanikiwa katika medani ya urembo nchini humo baada ya kuchukua nafasi ya pili katika mashindano ya malkia wa urembo nchini Tanzania mwaka 2006.
Anapoulizwa kuhusu swala la urembo yeye hutabasamu tu, akionesha mwanya uliopo kati ya meno yake, hali kadhalika kidoti cheusi kinachoshirikishwa na urembo kilichopo usoni mwake.
Sio vigumu kwa mtu anayemtafuta mkuu huyu wa wilaya miongoni mwa umati kumkosa kutokana na muonekano .
Vilevile bi Joketo ni miongoni mwa vijana maa...