Saturday, March 15

Kimataifa

Kenneth Kaunda – Mwana wa Afrika aliyekuwa na ushawishi ndani na nje ya Zambia
Kimataifa

Kenneth Kaunda – Mwana wa Afrika aliyekuwa na ushawishi ndani na nje ya Zambia

Kenneth Kaunda alikuwa ni mmoja wa viongozi waasisi wa Afrika mpya, wakati nchi yake ilipoondokana na ukoloni na kuwa taifa huru. Kiongozi huyu ambaye alikuwa na haiba ya uchangamfu, alisifiwa kama kiongozi aliyekuwa na msukumo wa kisasa katika bara licha ya kwamba mwanzoni aliikataa dhana ya demokrasia ya vyama vingi. Akiwa mwana wa Afrika aliyejitolea, alianza kazi ya kuijenga Zambia mpya, huru kuamua njia yake katika masuala ya kimataifa. Lakini usimamizi duni wa uchumi ulisambabisha umaarufu wake kushuka, na akaondolewa madarakani baada ya kushindwa kwa kura wakati uchaguzi huru ulipofanyika mwaka 1991. Kenneth David Kaunda alizaliwa tarehe 28 Aprili 1924 katika kituo cha wamishonari karibu na mpaka baina ya Rhodesia Kaskazini (Zambia ya sasa) na Congo. ...
Kuanzia Air Force One hadi ‘The Beast’ – Fahamu ulinzi wa aina yake anaopatiwa rais wa Marekani ziarani
Kimataifa

Kuanzia Air Force One hadi ‘The Beast’ – Fahamu ulinzi wa aina yake anaopatiwa rais wa Marekani ziarani

Rais wa Marekani Joe Biden amewasili nchini Uingereza katika ziara yake ya kwanza rasmi Ulaya. Ni kituo chake cha kwanza katika ziara ya siku nane huko Ulaya. Atahudhuria mkutano wa viongozi wa G7 mjini Cornwall na kukutana na Malkia kabla ya kuvuka na kuhudhuria shughuli zingine rasmi- ikiwa ni pamoja na kongamano lake la kwanza la Nato akiwa rais, na kumalizia ziara yake kwa kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Geneva. Safari ya Bw. Biden inajumuisha mambo mengi. Rais wa Marekani huandamana na usafiri maalum utakaomsaidia kutoka sehemu moja hadi nyingine, ardhini na angani. Na hakuna cha kushangaza zaidi kuliko ndege ya rais ya - Air Force One. Ndege hiyo ilitua RAF Mildenhall mjini Suffolk siku ya Ju...
EURO 2020: Mambo Matano muhimu kuhusu michuano hiyo
Kimataifa, Michezo

EURO 2020: Mambo Matano muhimu kuhusu michuano hiyo

Ilikuwa mwaka, miezi na sasa zinahesabika dakika kabla ya kuanza kwa Mashindano ya Euro 2020 Juni 11 mpaka Julai 11 mwaka huu. Mashindano haya yalikuwa yafanyike Juni 12 mpaka Julai 12 mwaka jana lakini yaliahirishwa kwa sababu ya uwepo wa janga la Corona. Jumla ya timu 24 zitashiriki mashindano hayo katika mechi 51 zitakazopigwa katika majiji 11 ya nchi za Ulaya, hata hivyo haifahamika ni kiasi gani cha mashabiki wataruhusiwa kuingia viwanjani kushuhudia michuano hiyo, kutokana na janga la Corona kuendelea katika maeneo mbalimbali ya bara hilo. Kwa mara ya kwanza pia michuano yam waka huu itatumia usaidizi wa video kwenye maamuzi (VAR). 1: Kundi gumu zaidi 'kundi la Kifo' Yapo makundi sita ya timu nne ne kila kitu, ambapo kundi gumu zaidi linatajwa kuwa ni...
Kifaru amesafiri kutoka Taiwan hadi Japan kutafuta mchumba
Kimataifa

Kifaru amesafiri kutoka Taiwan hadi Japan kutafuta mchumba

Ungefikiria ni binadamu pekee ambaye angeweza kufanya safari yamwendo mrefu kutafuta mpenzi au hata mapenzi .Lakinio sio kwa sababu hata wanyama kumbe wanahitaji mapenzi pia. Kifaru mweupe wa miaka mitano amesafiri kutoka Taiwan hadi Japani - yote hayo yakiwa ni sehemu ya kumtafuta mpenzi. Kifaru huyo kwa jina Emma ameanza kuishi Japani katika hifadhi ya wanyama ya Tobu, pamoja na kifaru wa miaka 10, Moran. Kifaru huyo alichaguliwa kati ya kundi la vifaru 23 watakaopelekwa Japani kwasababu ya haiba yake huku wafanyakazi wakisema kwamba "ni nadra sana kwake kuanza kupigana na wengine". Kupelekwa katika hifadhi ya wanyama ya Japani ni jaribio la kuongeza idadi ya vifaru weupe barani Asia. Vifaru mweupe wanachukuliwa kuwa katika hatari ya kutoweka, kulin...
Mgogoro wa Tigray-Ethiopia: Baa la njaa lililosababishwa na binadamu
Kimataifa

Mgogoro wa Tigray-Ethiopia: Baa la njaa lililosababishwa na binadamu

"Sasa hivi Tigray kuna ukame.", Mratibu wa masuala ya dharura wa Umoja wa mataifa Mark Lowcock, ameelezea kwa uwazi kabisa hali ilivyo huko kaskazini mwa Ethiopia, Alhamisi. Katika taarifa yake - iliyotolewa wakati wa majadiliano ya mkutano wa G7 iliangazia tathmini ya mgogoro huo iliyotolewa na shirika la utoaji chakula la Umoja wa Mataifa. Katika ripoti yake inakadiriwa kuwa watu 353,000 huko Tigray walikuwa katika awamu ya 5 ya janga hilo na milioni 1.769 zaidi zimetengwa katika awamu ya 4 ya mpango huo. Hiyo ni namna tu ya kusema kwamba kuna "baa la njaa". Ingawa shirika hilo halikutumia neno hilo kwasababu za kisiasa - ingawa serikali ya Ethiopia ingepinga hilo. Pia nyuma ya idadi hiyo, kuna ukiukaji wa haki za binadamu uliotokea. Idadi kubwa ...