Sunday, October 20

Kitaifa

Dk. Hussein Ali Mwinyi awaapisha wakuu wa Mikoa wapya.
Kitaifa

Dk. Hussein Ali Mwinyi awaapisha wakuu wa Mikoa wapya.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka Wakuu wa Mikoa wapya wa Zanzibar kuwa na utaratibu maalum unaotambulika wa  kusikiliza kero za wananchi  pamoja na kuzitafutia ufumbuzi. Dk. Mwinyi ametoa ushauri huo leo Ikulu jijini Zanzibar katika hafla ya kuwaapisha Wakuu wa Mikoa wapya, watakaohudumu katika Mikoa mitano ya Zanzibar. Walioapishwa ni  Ayoub Mohamed Mahamoud Mkoa Kaskazini Unguja, Rashid Hadid Rashid (Kusini Unguja), Idrissa Kitwana Mustafa (Mjini Magharibi), Salama Mbarouk Khatib (Kaskazini Pemba) pamoja na Mattar Zahor Masoud , mkoa wa Kusini Pemba.     Amesema viongozi hao wana jukumu la kuandaa utaratibu maalum utaowawezesha wananchi kuwasilisha kero mbali mbali zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi wa...
SOS yakabidhi saruji na bati kwa familia 38.
Kitaifa

SOS yakabidhi saruji na bati kwa familia 38.

  SHIRIKA lisilo la kiserikali Zanzibar SOS limekabidhi mifuko 623 ya saruji na bati 100 zikiwa na thamani ya Zaidi ya shilingi Milioni 11, kwa Familia 38 Zilizomo katika mpango wa kuimarisha familia unaosimamiwa na shirika hilo. Akikabidhi msada huo kwa familia hizo huko Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mjumbe wa bodi ya Shirika la SOS Zanzibar Dk.Issa Seif Salim alisema lengo la kukabidhi msaada huo ni kuwalinda watoto na kuishi katika mazingira mazuri. Alisema familia zinapokuwa katika mazingira mazuri ya makaazi, basi hata watoto nao wataishi katika mazingira mazuri na kupata muda mzuri wa kusoma masomo yao. Aidha amjumbe huyo wa bodi alisema SOS ipo mstari wa mbele katika kuwalinda na kuwapa maisha bora watoto, ili kufikia malengo hayo shirik...
Waziri wa habari awataka vijana .
Kitaifa

Waziri wa habari awataka vijana .

WAZIRI wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Mwita, amewataka vijana kisiwani Pemba kuvifanyia kazi vyarahami walivyokabidhiwa, kwa kutafuta tenda za ushonaji wa nguo ili viweze kuwasaidia katika masiha yao. Alisema vyarahani havipaswi kukaa tu baada ya kufungwa, badala yake wanapaswa kuvitumia katika ushonaji wa vitu mbali mbali ili fedha itakayopatikana iweze kutengenezea hata ofisi yo. Aliwayeleza hayo wakati alipokua akizungumza na vijana wa ushoni wa wilaya ya wete, huko katika ofisi za ushoni benjamini mkapa ya zamani wete. Aidha waziri huyo alitoa wiki mbili kwa ugozi wa kikundi hicho kuanza kazi ya ushonaji, huku akiwataka kutafuta tenda kwenye maskuli kwa sasa kwa ajili ya ushoni wanguo za wanafunzi na mambo mengine. “Serikali ya Mapinduzi imeweza ku...
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar: Vijana kuanzia sasa tieni nia ya kukataa kuwa waathirika wa Virusi vya Ukimwi.
Kitaifa

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar: Vijana kuanzia sasa tieni nia ya kukataa kuwa waathirika wa Virusi vya Ukimwi.

Na.Othman Khamis.OMPR. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Hemed Suleiman Abdulla wakati akiwataka Vijana kuanzia sasa watie nia ya kukataa kuwa waathirika wa Virusi vya Ukimwi, Jamii lazima ishirikiane kulilinda kundi hilo ili liendelee kubakia salama. Alisema utafiti unaonyesha kuwa Vijana wenye umri baina ya miaka 15 hadi 24 bado wanaongoza katika kupata maambukizo mapya ya Virusi vya Ukimwi kila Mwaka kwa asilimia 50% ya Watu wote changamoto ambayo jitihada za makusudi zinahitajika katika kupambana nayo. Akizungumza katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani  hapo katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Mh. Hemed Suleiman Abdulla alisema bila ya kuwa na Vijana wenye Afya nzuri, wachapa Kazi, ile dhamira ya Serikali isemayo yajayo ni neema tupu itabak...
Mbunge wa  Kiwani  Rashid Abdalla Rashid, amekabidhi gari la kubebea wagonjwa (AMBULANCE).
Kitaifa, Siasa

Mbunge wa Kiwani Rashid Abdalla Rashid, amekabidhi gari la kubebea wagonjwa (AMBULANCE).

  NDANI ya siku 20 tokea kula kiapo Bungeni, hatimae mbunge wa Jimbo la Kiwani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba Rashid Abdalla Rashid, amekabidhi gari la kubebea wagonjwa (AMBULANCE) kwa wananchi wa jimbo hilo likiwa na thamani ya shilingi Milioni 32,000,000/=. Gari gilo ambalo litaweza kutoa huduma kwa kuwafikisha wagonjwa katika vituo vya afya kwa lengo la kupata huduma za matibabu pale wanapopatwa na tatizo. Akizungumza katika makabidhiano ya gari hilo kwenye uwanja wa mpira Mauwani, mbunge huyo alisema CCM ikiahidi inatekeleza tena kwa vitendo na sio kumumunya maneno. Alisema kwanza ameanza na sekta ya afya ambayo ndio sekta muhimu katika jamii, kwani gari hiyo itatoa huduma katika shehia zote zilizomo ndani ya jimbo hilo. “Katika Jimbo letu kuna vikundi vi...