Saturday, October 19

Kitaifa

MBUNGE wa jimbo la Gando kupitia CCM Salim Mussa Omar, aungana na wanachama wa jimbo hilo, katika usafi
Kitaifa, Siasa

MBUNGE wa jimbo la Gando kupitia CCM Salim Mussa Omar, aungana na wanachama wa jimbo hilo, katika usafi

NA SAID ABRAHMAN.   MBUNGE wa jimbo la Gando kupitia CCM Salim Mussa Omar, ameungana na wanachama wa jimbo hilo, katika usafi wa eneo ambalo linatarajiwa kujengwa kwa Ofisi ya Mbunge wa jimbo.   Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM, waliojitokeza katika usafi huo katika Kijiji cha Minyenyeni jimbo la Gando, alisema kuwa tayari bajeti ya jengo hilo imekamilika.   Alisema kuwa lengo la kujenga Ofisi hiyo ni kuwaondoshea adha wananchi wake, wakati wa kukutana nao ili waweze kumueleza shida zao zinazowakabili katika jimbo lao. Salim alifahamisha kuwa wanajenga Ofisi hiyo, kwa mara ya kwanza tokea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama hapa nchini, hakuna Mbunge hata mmoja aliyethubutu kujenga Ofisi ya Mbunge ndani ya jimbo hilo.   "Tokea kuasisiw...
MBUNGE wa jimbo la Gando amekabidhi vifaa vya maji vyenye thamani ya Tsh  6,800,000/.
Kitaifa

MBUNGE wa jimbo la Gando amekabidhi vifaa vya maji vyenye thamani ya Tsh 6,800,000/.

  NA SAID ABRAHMAN.   MBUNGE wa jimbo la Gando kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Salim Mussa Omar, amekabidhi vifaa vya maji kwa ajili ya Kijiji cha Chozi Wilaya ya wete vyenye thamani ya Tsh 6,800,000/. Mradi huo utahudumia wananchi wapatao 1500 wa Kijiji hicho, ambapo kwa muda mrefu wamekuwa wakihangaika na tatizo la upatikanaji wa maji. Akikabidhi vifaa hivyo Mbunge huyo, aliwataka wananchi hao kuulinda mpira huo, ili usiweze kuharibiwa na wale wasiopenda maendeleo, huku akiwahakikishia  wananchi hao kuwa ataendelea kuwasaidia kwa kila hali itakapokuwa vizuri . “Sisi viongozi wenu wa majimbo kazi yetu ni kuunga mkono juhudi za serikali, kwa kuwafikishia maendeleo leo tumetoa mpira huu, kazi iliyobaki ni yenu ya kulinda miundombinu hiyooo”alisema. Aidha alisem...
Makamo wa pili atoa agizo kwa wizara ya afya Pemba.
Kitaifa

Makamo wa pili atoa agizo kwa wizara ya afya Pemba.

  MAKAMU wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, amemuagiza Mkurugenzi mkuu wa Bohari ya dawa Zanzibar kuharakisha utaratibu wa upatikanaji wa dawa katika bohari kuu ya dawa Pemba. Alisema bohari ya dawa Pemba imegharimu fedha nyingi na kufunguliwa karibuni, itakua haina maana ya kasi yote iliyofanywa na serikali ikaendelea kubeba gharama za lazima kuchukuliwa dawa Unguja na kuletwa pemba. Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar alitoa agizo hilo baada ya kutembelea maeneo mbali mbali ya hospitali ya Wilaya ya Micheweni, pamoja na kupokea changamoto za wafanyakazi wa hospitali hiyo katika ziara yake ya siku tatu kisiwani hapa. “Afisa Mdhamini kwa kushirikiana na mkurugenzi Tiba, hakikisheni dawa zote zinapatikana katika bohari ya dawa Pemba, sio tena kuagiza kutoka Un...
Wabunge wapya wasaidia vifaa hospital ya Wete.
Kitaifa

Wabunge wapya wasaidia vifaa hospital ya Wete.

  MBUNGE wa Jimbo la Gando Salum Mussa Omar na Mbunge wa Jimbo la Kojana Hamad Hassan Chande, wamekabidhi vifaa mbali mbali pamoja na Fedha taslimu shilingi Milioni 1.2, kwa uongozi wa Hospitali ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba. Vifaa hivyo vilivyokabidhiwa na wabunge hao, ni pamoja na mafeni, boks za Taizi, Glavu na dawa za usafi na kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya ununuzi wa AIC. Makabidhiano hayo yaliofanyika katika hospitali hiyo Wete, ikishuhudiwa na watendaji mbali mbali wa Hospitali na baadhi ya wananchi waliofika hospitalini hapo kuwaona jamaa zao. Akizungumza katika hafla hiyo, mbunge wa Jimbo la Gando Salumu Mussa Omar alisema licha ya kukabidhi vifaa hivyo, lakini haridhishwi na hali ya mazingira ya hospitali hiyo ilivyo, pamoja na kutokufanya kazi kwa baad...
Mjumbe wa Kamat Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Mh. Hemed Suleiman Abdulla zungumza na Wana CCM na Wananchi wa Jimbo la Kiwani
Kitaifa, Siasa

Mjumbe wa Kamat Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Mh. Hemed Suleiman Abdulla zungumza na Wana CCM na Wananchi wa Jimbo la Kiwani

Mjumbe wa Kamat Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Mh. Hemed Suleiman Abdulla alisema Viongozi Wakuu watalazimika kuchukuwa maamuzi magumu katika kuona nidhamu ya Serikali katika kutoa Huduma kwa Wananchi inarejea katika uhalisia wake. Alisema wakati Serikali inaendelea kupanga safu ya Utendaji katika uwajibikaji wake baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu Wananchi wanapaswa kuunga mkono jitihada hizo ili yale matarajio yao yaweze kufikiwa kwa ufanisi na uharaka uliokusudiwa. Mh. Hemed Suleiman Abdulla alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na Wana CCM na Wananchi wa Jimbo la Kiwani  katika Mkutano Maalum ulioandaliwa wa kumpongeza kwa Kuteuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Ali Mwinyi kushika wadhifa huo. Alisema Chama cha Mapinduzi mba...