MBUNGE wa jimbo la Gando kupitia CCM Salim Mussa Omar, aungana na wanachama wa jimbo hilo, katika usafi
NA SAID ABRAHMAN.
MBUNGE wa jimbo la Gando kupitia CCM Salim Mussa Omar, ameungana na wanachama wa jimbo hilo, katika usafi wa eneo ambalo linatarajiwa kujengwa kwa Ofisi ya Mbunge wa jimbo.
Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM, waliojitokeza katika usafi huo katika Kijiji cha Minyenyeni jimbo la Gando, alisema kuwa tayari bajeti ya jengo hilo imekamilika.
Alisema kuwa lengo la kujenga Ofisi hiyo ni kuwaondoshea adha wananchi wake, wakati wa kukutana nao ili waweze kumueleza shida zao zinazowakabili katika jimbo lao.
Salim alifahamisha kuwa wanajenga Ofisi hiyo, kwa mara ya kwanza tokea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama hapa nchini, hakuna Mbunge hata mmoja aliyethubutu kujenga Ofisi ya Mbunge ndani ya jimbo hilo.
"Tokea kuasisiw...