Saturday, October 19

Kitaifa

Makamo wa Pili awajia juu wakandarasi ZRB na ZBC.
Kitaifa

Makamo wa Pili awajia juu wakandarasi ZRB na ZBC.

  MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, amewaonya wakandarasi wanaojenga jingo la Ofisi za ZRB Gombani na Ofisi za ZBC TV Mkoroshoni, kuacha tabia ya kutafuta sababu ya kwamba mvua ndio kigezo kilichopeleka kuchelewa kwa majengo hayo kumalizika kwa wakati. Alisema tabia hiyo ya wakandarasi wanapopewa kazi za ujenzi kwa majengo ya serikali mwisho wake umefika, bali wanapaswa kujega kulingana na mikataba ya ujenzi waliosainiana na wenyeji wao. Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, alitoa kauli hiyo baada ya kutembelea majengo hayo kwa nyakati tafauti, katika mwendelezo wa Ziara yake Kisiwani Pemba. Akizungumzia jingo la Ofisi za ZRB Gombani, alimtaka mkandarasi huyo kuhakikisha jingo hilo analimaliza ndani ya muda uliopangwa, wakati...
Jamii iendelee  kudumisha amani na utulivu nchini.
Kitaifa, Sheria

Jamii iendelee kudumisha amani na utulivu nchini.

  WADAU wa uchaguzi Kisiwani Pemba wametakiwa kuishajihisha jamii kuendelea kudumisha amani na utulivu nchini katika kipindi hichi ambacho Taifa linatoka katika uchaguzi mkuu. Uchaguzi umemaliza na serikali iko madarakani hivyo lililopo kwa sasa ni kudumisha amani na utulivu na kusahau yaliyopita kwani ukizingatia kuna maisha baada ya uchaguzi. Akitowa mada juu  umuhimu wa kulinda amani kwa wadau hao uliofanyika ukumbi wa Maktaba Chake chake kaimu mratibu wa kituo cha huduma za sheria tawi a Pemba Safia Saleh Sultan alisema kila mmoja ana haki ya kulinda amani na kuondosha ugomvi ,vita na mifarakano katika nchi ili kila mmoja aweze kuendesha maisha kwa salama . Alifahamisha kuwa ili amani iweze kudumu vyema ni vizuri kuanzia ndani ya familia na baadae kwenye shehia, wi...
Watu wenye Ulemavu  ni mfano bora katika Uwajibikaji.
Kitaifa

Watu wenye Ulemavu ni mfano bora katika Uwajibikaji.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inapendelea kuona Watu wenye Ulemavu Nchini wanakuwa mfano bora katika Uwajibikaji ndani ya Taifa hasa ikizingatiwa kwamba jitihada zao wanazochukuwa zimelenga kujikomboa katika harakati zao za Kimaisha za kila siku. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Hemed Suleiman Abdulla alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na Uongozi wa Idara ya Watu Wenye Ulemavu hapo Makao Makuu ya Idara hiyo yaliyopo Migombani wakati akiwa kwenye ziara ya kuzitembelea Idara na Taasisi zilizo chini ya Afisi yake. Alisema Watu Wenye Ulemavu wana nguvu na uwezo mkubwa wa kufanya kazi kama walivyo Watu wengine kwenye uwajibikaji, lakini kinachohitajika kwa Jamii inayowazunguuka ni kukubali kuwapa dhamana kwa mujibu wa Maarifa, Elimu na Vipaji walivyobarikiwa. Hata hivyo Mh. Hem...
Ahukumiwa kwenda chuo cha mafunzo.
Kitaifa, Sheria, Wanawake & Watoto

Ahukumiwa kwenda chuo cha mafunzo.

  Kijana  Khamis  Shaib Khatib  mwenye umri wa miaka  24 mkaazi  wa Kizimbani Wete Pemba ahukumiwa kwenda  chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka  saba  [7]  na kutozwa faini ya shilingi laki mbili za kitanzania baada   ya  kupatikana na hatia ya kumbaka  msichana wa miaka kumi na tatu [13]. Hukumu hiyo imesomwa na  hakimu  Abdala  Yahya  Shamuhun  baada  ya kuona ushahidi uliotolewa mahakamani hapo unaridhisha. Hakimu huyo alimtaka mshitakiwa huyo kwenda kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka  saba [7] na kutozwa fidia ya shilingi laki mbili baada ya mahakama kumtia hatiani kwa kosa la kubaka. “Mtuhumiwa umepatikana na hatia kwa  kosa la  kubaka  utatumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka  saba[7]” alisema shamuhun. Kabla ya kusomewa shitaka lake hilo mshitaki...
Makamo wa Rais wa Zanzibar atua Pemba.
Kitaifa, Siasa

Makamo wa Rais wa Zanzibar atua Pemba.

  MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, amewapongeza wananchi wa mikoa miwili ya Pemba, kwa mapokezi yao mazuri kwani hali hiyo inaonyesha heshima kubwa kwa Rais Dk Hussein Mwinyi kumuamini katika utendaji wake wa kazi. Alisema Tayari Rais ameshaanza kupanga serikali yake na mwelekeo wa serikali hiyo ya awamu ya nane, kila mtu ameshaanza kuona kwani Imekusudia kuwabadilisha wananchi wa Zanzibar. Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar aliyaeleza hayo wakati alipokuwa akiwahutubia wananchi wa mikoa miwili ya Pemba, mara baada ya kuwasili Kisiwani hapa kwa mara ya kwanza tokea kuteuliwa kwake na Rais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi. Alisema kasi ya serikali hiyo imeanza hivyo mashirikiano na uwajibikaji ndio kitu muhimu, kwani hawako tayari kuona wabadhili...