Jamii yatambuweni maradhi yasiyopewa kipaumbele.
NA MARYAM SALUM, PEMBA.
JAMII Kisiwani Pemba imetakiwa kutambua yapo maradhi yasiyopewa kipaombele, ambayo yanaweza kumpata kila mtu na kila rika, hivyo ni vyema kuchukua tahadhari, katika kujikinga na maradhi hayo.
Hayo yalielezwa na Mratibu wa kitengo cha maradhi yasiyopewa kipaombele Kisiwani Pemba, Dk Saleh Juma Mohamed wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi Ofisini kwake Mkoroshoni Chake Chake.
Alisema wananchi waliowengi hufikiria kwamba maradhi hayo huwapata watoto wadogo tu, jambo ambalo sio sahihi kwani maradhi hayo huwapata watu wa rika lolote.
“Watoto wadogo ndio wanaonekana kupatwa na maradhi ya mripuko, kwa sababu ndio ambao wanaonekana mara nyingi kucheza ama kuzurura ovyo, kwenye mazingira yasiyokuwa salama juu ya afya zao,” alisem...