Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe Riziki Pembe Juma amkabidhi Ofisi Waziri wa Elimu na mafunzo ya Amali, Mhe Simai Mohammed Said.
Na Mwandishi wetu
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imefanya makabidhiano ya ofisi kwa aliekuwa Waziri wa Wizara hiyo Mhe Riziki Pembe Juma ambae kwa sasa ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi na kumkabidhi Mhe Simai Mohammed Said.
Hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika ukumbi wa Wizara hiyo Mazizini Mjini Unguja.
Akizungumza baada ya makabidhiano hayo aliekuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma ameushukuru uongozi wa Wizara hiyo kwa malezi na ushirikiano mkubwa waliompa katika kipindi chote cha uongozi wake ndani ya Wizara hiyo na kuweza kuzalisha viongozi walioweza kupanda kutoka Naibu Waziri na kuwa Waziri kamili.
Aidha Mhe Riziki ameiahidi Wizara hiyo kuendelea kuwapa ushirikiano wa k...