Mwili wa aliekuwa askari wa kikosi cha KVZ wapatikana pamoja na bunduki.
MWANDISHI WETU, PEMBA.
JESHI la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba limefanikiwa kuupata mwili wa aliekuwa askari wa kikosi cha KVZ Khalfan Junedi mwenye miaka 25 aliuwawa baada ya wiki tatu zilizopita huko eneo la Ngwachani Wilaya ya Mkoani.
Pamoja na mwili huo pia lilifanikiwa kuipata bunduki aina ya AK47 katika eneo la Ngwachani Novemba 12 majira ya saa 2:00 usiku ambayo magazine yake ikiwa na risasi 21.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Ahmed Khamis Makarani amesema mwili huo ulipatika katika kijiji cha chonga kwenye bonde la Kisitu mbwa.
Alisema kuwa, Novemba 15 walifanikiwa kuupata mwili wa askari huyo baada ya kumkamata mtu mmoja anaejulikana kwa jina la Ussi Foum Machano mkaazi wa Ngwachani, ambae aliwapeleka ...