Saturday, October 19

Kitaifa

Wananchi kuchukua tahadhari juu ya Kichocho.
Kitaifa

Wananchi kuchukua tahadhari juu ya Kichocho.

WANANCHI Kisiwani Pemba wametakiwa kuendelea kujitahidi kuchukua tahadhari juu ya maradhi ya Kichocho, katika kipindi hiki cha mvua za Vuli zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali. Wito huo umetolwa na mratib wa kitengo cha Maradhi yasiopewa Kipau Mbele Pemba, Dk.Saleh Juma Mohamed huko Ofisini kwake mkoroshoni Chake Chake Pemba. Dk.Saleh alisema katika kipindi hiki cha mvua za vuli zinazoendelea kunyesha, vizuri wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kubwa juu ya maradhi hayo, kwa kuacha kutumia maji katika madimbwi au kwenye mabwa badala yake kutumia maji ya mfereji kwa shuhuli zao mbali mbali. Alisema maradhi ya kichocho ni miongoni mwa maradhi yanayo uwa kidogo kidogo kwani, baktiri wa maradhi hayo anayojulikana kwa jina la Bilharzia(Schistosomiasis) hushi katika m...
Matokeo ya uchaguzi Tanzania 2020: Je, nani na nani kuingia Baraza jipya la Mawaziri wa Rais Magufuli?
Kitaifa

Matokeo ya uchaguzi Tanzania 2020: Je, nani na nani kuingia Baraza jipya la Mawaziri wa Rais Magufuli?

Saa 1 iliyopita   Leo Ijumaa rais mteule wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuhutubia Bunge la nchi hiyo katika jiji la Dodoma lililopo katikati ya taifa hilo la Afrika mashariki ambayo itazindua rasmi Bunge la 12. Tangu alipoapishwa Novemba 5 mwaka huu kuliongoza taifa hilo katika kipindi cha pili wa miaka mitano 2020-2025, hivi karibuni akiwa jijini humo mbele ya wabunge wa CCM alibainisha kuwa hana mpango wa kuteua wakuu wapya wa mikoa, wilaya, makatibu wakuu wa wizara, wakurugenzi wa Halmashauri na taasisi mbalimbali za umma badala yake amewataka waendelee kuchapa kazi kama walivyoanza pamoja na hivyo wamalize wakiwa wamoja. Mbali ya hilo, rais huyo anakabiliwa na kibarua kizito cha kuunda baraza jipya la mawaziri la serikali yake, huku baadhi ya viongoz...
Kiwango cha madini ya uranium cha Iran kimepita mara 12 ya kiwango kinachohitajika, yasema IAEA
Biashara, Kitaifa

Kiwango cha madini ya uranium cha Iran kimepita mara 12 ya kiwango kinachohitajika, yasema IAEA

Shirika la Kimataifa la nishati ya atomiki (IAEA) limesema kuwa akiba ya uranium ya kiwango cha chini imefikia kilo 2,442.9 mwezi huu. Iran inasisitiza kuwa mipango yake ya nyuklia ni ya malengo ya amani tu. IAEA pia ilisema kuwa maelezo ya Iran kwa ajili ya uwepo wa nyuklia katika eneo ambalo haijalitangaza wazi ''sio ya kuaminika'' Kwenye ujumbe wa Twitter, balozi wa Iran katika IAEA, Gharib Abadi, alisema kuwa "kauli zozote za haraka zinapaswa kuepukwa", akiongeza kuwa: "mazungumzo yanaendelea kwa lengo la kukamilisha azimio la suala hilo ." Katika ripoti yake ya hivi karibuni, iliyosambazwa kwa wanachama, IAEA kutambua eneo ambako ilipata vifaa vya nyuklia. Chanzo ambacho hakikutajwa kililiambia shirika la habari la AFP kwamba hapakuwa na kiashiria chochote kwamba h...
Wizara yakabidhi vifaa vya ushoni kwa vijana.
Kitaifa

Wizara yakabidhi vifaa vya ushoni kwa vijana.

WIZARA ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Pemba, imekabidhi vifaa mbali mbali vya ushoni kwa viongozi wa Wilaya nne za Pemba, kwa ajili ya vijana waliomaliza mafunzo ya ushoni Kisiwani hapa, kwa lengo la kuendelea ujuzi wao huo pamoja na kujikwamua na umasikini. Vifaa hivyo vilivyokabidhiwa ni pamoja na vyarahani 76 Butterfly na Sinja, overlock 12, Pasi 20, Mikasi 123, trpu 72 na Juki 12 ili kuwasaidia vijana hao kufikia malengo yao ikiwemo kushona bila ya usumbufu. Akitoa maelezo juu ya utoaji wa msaada huo kwa vijana, afisa Mdhamini Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Pemba Fatma Hamad Rajab, alisema utoaji wa mssada huo kwa vijana umetokana na mipango madhubuti ya Rais Mstaafu wa Zanzibar Dk Shein, katika kuwasaidia vijana wa Zanzibar kupitia program ya vijana. Al...
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi awasili Dodoma kuhudhuria ufunguzi wa Bunge la 12 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kitaifa

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi awasili Dodoma kuhudhuria ufunguzi wa Bunge la 12 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyiamewasili Jijini Dodoma leo kwa ajili ya kuhudhuria uzinduzi wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika uwanja wa ndege wa Dodoma, Rais Dk. Hussein amepokewa na viongozi mbali mbali wa Serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk. Binilith Mahenge. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Joseph Magufuli anatarajiwa kulizindua Bunge hilo la 12 mnamo majira ya asubuhi hapo kesho Ijumaa. Kwa kawaida Mkutano wa Kwanza wa Bunge jipya kama huo huwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania analihutubia Bunge kwa maana ya kuweka dira kwenye Serikali yake kwa miaka mitano inayokuja na utekelezaji wa Ilani kadri anavyoona inafaa. Shughuli hiyo ya uzinduzi wa Bunge itatangu...