Makamu wa Pili wa Rais Mteule wa Zanzibar Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdallah anena.
Makamu wa Pili wa Rais Mteule wa Zanzibar Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdallah alisema Wananchi wa Zanzibari wanapaswa kujenga matumaini makubwa kwa Serikali Mpya itakayojizatiti kuwajibika ipasavyo katika kuwaletea maendeleo.
Alisema uwajibikaji huo utakaozingatia kutotoa nafasi kwa Watendaji wenye tabia ya kukumbatia dhambi, ubadhirifu, uzembe pamoja na wizi ndio mfumo utakaotumiwa na Serikali chini ya usimamizi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Ali Mwinyi.
Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdallah alitoa kauli hiyo akizungumza na Wanahabari muda mfupi baada ya kula kiapo cha Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kufuatia Uteuzi uliofanywa na Rais wa Zanzibar na hapo hapo Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mh. Zubeir Ali Maulid kuli...