Shuhuli za kijamii zarejea Pemba..
SHUHULI mbali mbali za kijamii ambazo zilisimama tokea Oktoba 27 mwaka huu, katika maeneo mbali mbali ya Kisiwa cha Pemba sasa zimerudi katika hali yake asili.
Shuhuli hizo ikiwemo huduma za usafiri wa barabarani, maduka ya biashara, pamoja na wafanya biashara mbali mbali wadogo wadogo nao wamejitokeza kwa wingi katika mji wa Chake Chake.
Shuhuli hizo zilisimama kwa kupisha kura ya mapema ya Oktoba 27 na upigaji wa Kura Oktoba 28 mwaka huu, ili kutoa nafasi kwa wananchi kutumia haki yao ya kidemokrasia ya kuchagua viongozi wanaowataka.
Mwandishi wa habari hizi alipata nafasi ya kuzungumza na baadhi ya wananchi, walisema kwa sasa hakuna haja ya kuendelea kusimama kwa shuhuli za kijamii, wakati uchaguzi umeshamalizika na washindi wameshatangazwa.
Khamis Ali Mwalimu ...