Saturday, October 19

Kitaifa

Kitaifa

Shuhuli za kijamii zarejea Pemba..

  SHUHULI mbali mbali za kijamii ambazo zilisimama tokea Oktoba 27 mwaka huu, katika maeneo mbali mbali ya Kisiwa cha Pemba sasa zimerudi katika hali yake asili. Shuhuli hizo ikiwemo huduma za usafiri wa barabarani, maduka ya biashara, pamoja na wafanya biashara mbali mbali wadogo wadogo nao wamejitokeza kwa wingi katika mji wa Chake Chake. Shuhuli hizo zilisimama kwa kupisha kura ya mapema ya Oktoba 27 na upigaji wa Kura Oktoba 28 mwaka huu, ili kutoa nafasi kwa wananchi kutumia haki yao ya kidemokrasia ya kuchagua viongozi wanaowataka. Mwandishi wa habari hizi alipata nafasi ya kuzungumza na baadhi ya wananchi, walisema kwa sasa hakuna haja ya kuendelea kusimama kwa shuhuli za kijamii, wakati uchaguzi umeshamalizika na washindi wameshatangazwa. Khamis Ali Mwalimu ...
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali atakayoiunda itashirikiana na vyama vya upinzani.
Kitaifa, Siasa

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali atakayoiunda itashirikiana na vyama vya upinzani.

  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali atakayoiunda itashirikiana na vyama vya upinzani vilivyokubali na kuridhishwa na matokeo ya urais yaliyotokana na uchaguzi mkuu uliofanyika octoba 28,mwaka huu. Ahadi hiyo aliitoa wakati akiwahutubia wananchi mara baada ya kuapishwa kuwa rais wa awamu ya nane wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar, katika hafla iliyofanyika uwanja wa Amani Unguja. Alisema anawapongeza wagombea wa vyama vya upinzania waliokubali matokeo ya uchaguzi na kuheshimu maamuzi ya wananchi na ninatoa ahadi ya kushirikiana nao katika serikali atakayounda. “Ndugu zangu ninawapongeza wagombea wenzangu kwa nafasi ya urais ambao wameyakubali matokeo ya uchaguzi na kuheshimu maamuzi ya wananchi na ninatoa ah...
Wawakilishi wateuliwa wanena.
Kitaifa, Siasa

Wawakilishi wateuliwa wanena.

  WAWAKILISHI wateule wa Majimbo Mbali Mbali Mkoa wa Kusini Pemba, wamesema kuwa sasa kazi iliyombele yao ni kuhakikisha wanatimiza kwa vitendo ahadi zote walizozitoa katika mikutano ya kampeni wakati wakiomba kura kwa wananchi. Wawakilishi hao amboa wameshinda katika majimbo yao ya uchaguzi na kuthibitishwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC na kupatiwa vyeti vya uthibitisho huo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, baada ya kumailiza kwa matokeo ya uchaguzi, walisema watahakikisha wanatekeleza yote walioyaahidi kwa wananchi wakati wakiwaomba kura. Mwakilishi mteule wa jimbo la Chonga Wilaya ya Chake Chake, Suleiman Massoud Makame alisema ushindi alioupata umetokana na kazi nzuri, iliyoifanya ya kuwaelimisha wananchi kuchagua CCM wakati wa kampeni. Aliwataka wan...
NGO’s zatakiwa kutambua wajibu wao kwa jamii.
Kitaifa

NGO’s zatakiwa kutambua wajibu wao kwa jamii.

MTANDAO wa Asasi za kiraia Pemba (PASCO) umezitaka NGOs Kisiwani humo, kutokujiingiza katika masuala ya kisiasa badala yake kutambua wajibu wao katika kusaidia jamii. Hayo yameelezwa na katibu Mkuu PASCO Sifuni Ali Haji, wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa kupitia uwasilishwaji wa Rasimu ya Mswaada wa sheria ya jumuiya zisizo za kiserikali, uliofanyika mjini chake chake. alisema sio jambo jema kwa wanajumuiya za asasi za kiraia kujishuhulisha na mambo ya kisiasa, katika kipindi hiki cha uchaguzi badala yake kujuwa majukumu yao katika jamii. Aidha aliwataka wanajumuiya kuhakikisha wanafuata sera, sheria na kanuni za jumuiya zao katika kuwasaidia wananchi, katika kuwapatia maendeleo. Akizungumzia kuhusu uwasilishwa...
Balozi Ramia awaaga wafanyakazi  Pemba.
Kitaifa

Balozi Ramia awaaga wafanyakazi Pemba.

WAZIRI wa Fedha na Mipango Zanzibar Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa, amewaaga rasmi wafanyakazi wa wizara yake Pemba, huku akiwataka wanafanyakazi hao kutambua kuwa wizara hiyo nimiongoni mwa wizara ngumu pamoja taasisi zake. Alisema taasisi zilizomo ndani wa wizara hiyo ni ngumu sana, lazima wanapaswa kufahamu kwamba ni kazi za umma na sio zao, hivyo wanapaswa kujitahidi wakati wa kutoa huduma kwa wateja wao. Waziri huyo aliyaekeza hayo katika sherehe ya wafanyakazi ya kumuaga waziri wao, baada ya kuwahudumia kwa muda mrefu na kufanyika katika ukumbi wa wizara hiyo Gombani. Alisema lazima wafanyakazi wawe katika mstari mmoja, kufanya kazi kwa uwaminifu, mashirikiano pamoja na kufanya kazi kwa kukinai na kuacha tama. “Tambuweni Wizara hii kuwa inavishawishi vingi lazima, kama...