Saturday, October 19

Kitaifa

Wawi wafunga kampeni.
Kitaifa, Siasa

Wawi wafunga kampeni.

  MWENYEKITI wa chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba Yussuf Ali Juma, amewataka wananchi na wananchama wa CCM Kisiwani Pemba, kutokujitokeza kwenda kupiga kura Oktoba 27 badala yake kubaki majumbani kwa siku hiyo. Alisema siku ya kupiga kura kwa wananchi wa Zanzibar ni Oktoba 28 ambayo imetangazwa kihalali na tume ya uchaguzi Zanzibar, kwani siku ya Oktoba 27 ni siku ya watu maalumu. Mwenyekiti huyo aliyaeleza hayo wakati alipokua akiwanadi wagombea wa CCM jimbo la Wawi, Mbunge, Mwakilishi na Udiwani katika mkutano wakufunga kampeni za jimbo hilo uliofanyika skuli ya Maandalizi Machomanne Chake Chake. Aidha aliwasihi wananchi kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kwenda kupiga kusa Oktoba 28 mwaka huu, pamoja na kuacha kuvaa sare za chama chochote cha siasa kwa siku h...
DK Mwinyi anena Kiwani.
Kitaifa, Siasa

DK Mwinyi anena Kiwani.

   IMEANDIKWA NA HABIBA ZARALI NA HAJI NASSOR, PEMBA. MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema iwapo wananchi wa Zanzibar watampa ridhaa ya kushika nafasi hiyo, ataimarisha huduma za afya, ili wananchi wapate uhakika wa matibabu. Dk. Mwinyi ameyasema hayo uwanja wa mpira Jimbo la Kiwani wilaya ya Mkoani, mkoa wa kusini Pemba, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni wa chama hicho, uliokuwa na lengo la kuwanadi wagombea wa CCM. Alisema, hayo ndio kipaumbele chake cha kwanza mara atapomaliza kuapishwa, kwani mambo hayo ni miongoni mwa mambo muhimu kwa wananchi. Alisema moja ya dhamira yake ya kugombea nafasi hiyo, ni kuwatumikia wananchi kwa moyo wa dhati, na ndio maana anakusudia kuimrisha huduma za afya. Alisema ata...
UNESCO yakutana na walimu.
Kitaifa

UNESCO yakutana na walimu.

SHIKIKA la Umoja wa Mataifa elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limewata walimu wa skuli za sekondari na msingi Wilaya ya Mkoani, kuyatumia vyema mafunzo ya stadi za maisha, Ukimwi, afya ya uzazi na elimu ya jinsia, ili kuweza kuwasaidia wanafunzi wao katika kufikia malengo yao ya kielimu. Hayo yameelezwa na mratibu wa miradi kutoka shirika la UNESCO Dar Esaalam Viola Muhangi, wakati alipokuwa akizungumza na walimu hao, kabla ya kuanza kwa mafunzo ya siku sita huko katika skuli ya Mohamed Juma Pindua Mkanyageni Wilaya ya Mkoani. Alisema mafunzo hayo ya ni muhimu sana kwa walimu katika kuwasaidia wanafunzi wao kuweza kufikia malengo yao ya kielimu, kwani wananfunzi wengi wamekuwa wakikatisha ndoto zao mapema. Alifahamisha kuwa wilaya ya mkoni ndio wilaya ya kwanza kwa Zanzibar ...
PBZ yawashukuru wateja wake.
Biashara, Kitaifa

PBZ yawashukuru wateja wake.

  UONGOZI wa Benk ya watu wa Zanzibar Tawi la chake Chake, umewashukuru wateja wake kwa kuendelea kuitumia kwa kueka amana zao katika benka hiyo. Kauli hiyo imetolewa na kaimu meneja wa benk hiyo Said Saleh Rashid, wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika kuadhimisha wiki ya wateja wa benk. Alisema wiki ya wateja wa benk huadhimishwa duniani kote, hivyo Pbz imeona kuungana na wateja wake, ili kuendeleza utoaji wa huduma bora na kuwa nao kutokana na mchango wao kwa benk hiyo. Kaimu meneja alifahamisha Pbz imeweza kuboresha huduma mbali mbali, kwa lengo la kuwarahisishia wateja wao kuweza kunufaika na huduma hizo. “Sisi leo tumeona ni bora kuwa pamoja na wateja wetu katika kuzimisha wiki ya wateja wa mabenk, siku hii huadhimishwa duniani kote, wa...
Mti mrefu kumbe upo Tanzania.
Kitaifa

Mti mrefu kumbe upo Tanzania.

  Mti mrefu barani Afrika uko Tanzania, ni kivutio watalii Mti mrefu zaidi Afrika kivutio kipya cha watalii Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro uliopo kaskazini mwa Tanzania, ni maarufu kwa shughuli za utalii. Kila mwaka watalii huja kwa lengo la kupanda Mlima Kilimanjaro. Lakini hivi sasa, watalii wamepata kivutio chengine mkoani humo. Hii ni baada ya serikali ya Tanzania kutangaza kuwepo kwa mti mrefu zaidi barani Afrika. Mti huu aina ya Mkukusu una urefu wa mita 81.5 na unaopatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA). Ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Dk. Andreas Hemps na mkewe wote kutoka nchini Ujerumani ndio waliobaini kuwepo kwa mti huo umbali wa mita 1600 kutoka usawa wa bahari baada ya utafiti uliohusisha nchi nyengine barani Afrika kwa kip...