Saturday, October 19

Kitaifa

Wanasayansi washindwa kufumbua fumbo la uwepo wa dhahabu nyingi duniani.
Kitaifa

Wanasayansi washindwa kufumbua fumbo la uwepo wa dhahabu nyingi duniani.

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES Maelezo ya picha, Mlipuko wa nyota kubwa angani huenda unachangia wingi wa dhahabu, lakini haitoshi Kila uchao kiwango cha dhahabu ambayo haijachimbwa kinaendelea kupungua duniani. Kiwango cha dhahabu ilichosalia duniani kinakadiriwa kuwa karibu tani 50,000, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na wanajiolojia wa Marekeni. Tafiti zilizofanywa awali zilibaini kuwa dhahabu haiwezi kukuzwa upya. Hata hivyo tafiti tofauti katika miaka ya hivi karibuni zimefichua kuwa kuna hifadhi kubwa ya dhahabu nje ya sayari ya dunia. Inasadikiwa kuwa kiwango hicho kikubwa cha dhahabu ambacho sio ya kawaida imewafanya wanasayansi kukuna vichwa kwa miaka kadhaa wakijaribu kutafuta inapatikana wapi hasa. Ripoti iliyotolewa wiki hii inaashiria kuwa kiwango c...
DK. Shein azindua barabara Ole-Kengeja.
Kitaifa

DK. Shein azindua barabara Ole-Kengeja.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amewataka wananchi na watumiaji wa brabara ya Ole- Kengeja, kufanya kila njia ili kuhakikisha wanaitunza kwa nguvu zao zote, barabara hiyo ili idumu kwa muda mrefu. Dk. Shein ameeleza hayo uwanja wa mpira Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, alipokuwa akizungumza na wananchi wa mikoa mwili ya Pemba, mara baada ya kuzindua barabara hiyo mpya yenye urefu wa kilomita 35. Alisema barabara ndio kichecheo kikubwa cha maendeleo ya wananchi kwa kule kuitumia kwa shughuli zao mbali mbali iwe ni usafirishaji mazao, hivyo suala la kuitunza ni jambo la lazima. Alisema, ujenzi wa barabara hiyo umetumia fedha nyingi, hivyo hakuna budi kuona upo umuhimuwa na ulazima wa kuitunza kwa wananchi, ili itumike na k...
DK. Shein azindua BOHARI ya dawa Pemba.
Kitaifa

DK. Shein azindua BOHARI ya dawa Pemba.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, amesema kujengwa kwa bohari ya kuhifadhia dawa kisiwani Pemba, litaondosha tatizo la uagiziaji dawa Unguja na kwamba Hospitali na vituo vya afya vyote Pemba vitachukuwa dawa katika bohari hiyo kwa wakati muwafaka. Alisema hayo ni mafanikio makubwa ambayo hayajawahi kufikiwa, hivyo wananchi na watendaji wanapaswa kulitunza na kulithamini, ili bohari hiyo inadumu kwa muda mrefu na kukidhi mahitaji wa dawa. Rais Dk.Shein aliyaeleza hayo mara baada ya kuzindua rasmi bohari ya kuhifadhia Dawa, huko Vitongoji Changuo Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kuisni Pemba. Aidha Dk Shein aliahidi kufanya kila linalowezekana, kuona dawa muhimu zinapatikana katika haospitali na vituo vyote vya afya, kwamba serikali ime...
Kuweka mazingira safi ni njia ya kujikinga na maradhi yakiwemo ya mripuko. Waziri Hamad.
Kitaifa

Kuweka mazingira safi ni njia ya kujikinga na maradhi yakiwemo ya mripuko. Waziri Hamad.

  Waziri wa Afya Zanzibar Mh. Hamad Rashid Mohammed amewataka wananchi kuongeza juhudi katika kuweka mazingira yao safi na salama ili kuepuka kushambuliwa na maradhi yatakayopelekea kuzorotesha afya zao na kurudi nyuma kimaendeleo. Muheshimiwa Hamad ametoa wito huo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi katika maadhimisho ya siku ya kunawa mikono duniani huko katika Ukumbi wa  Samail Gombani Kisiwani Pemba. Mh. Hamad amesema ili mafanikio zaidi yaweze kupatikana ni lazima wananchi wawe katika hali ya usafi wa mazingira yao huku wakidumisha amani iliyopo ili kila mmoja aweze kupata nafasi ya kufanya kazi kwa ufanisi. “siku zote uchafu ndio ambao unasababisha maradhi na watu wengi huugua kutokana na uchafu” alisema Mh. Hamad. Amesema mara nyingi kunapotokea maradhi ...
DK. Shein anena Micheweni.
Kitaifa, Siasa

DK. Shein anena Micheweni.

MAKAMU mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar, Dk.Ali Mohamed Shein amesema kazi kubwa iliyopo mbele inapaswa kufanywa na wanaccm, kwa kuhakikisha wakakirudisha tena madarakani chama cha Mapinduzi na dhambi ya wanahubiri ugomvi ni kuwanyima kura. Alisema uongozi hautaki mzaha au kujaribu, kwani wanaCCM wako makini sana ndio maana wakakamilisha utekelezaji wa ilani ya CCM ya miaka mitano iliyopita, na kufanikiwa katika mambo mengi ya maendeleo hata yakipimwa kwa kutumia mizani. Makamu huyo mwenyekiti wa ccm Zanzibar, ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi, aliyaeleza hayo katika uwanja wa Shamemata Micheweni, wakati akiwahutubia wananchi na wanaccm wa wilaya hiyo. Akizungumzia suala la Mapinduzi matukufu ya zanzibara ya 1964, ndio yaliyoleta uko...

Warning: file_get_contents(): http:// wrapper is disabled in the server configuration by allow_url_fopen=0 in /data/40/5/71/99/5397425/user/6768456/htdocs/portal/wp-content/plugins/xt-visitor-counter/xt-visitor-counter.php on line 48

Warning: file_get_contents(http://api.xtrsyz.org/xt-visitor-counter/default.php?domain=www.pembapress.club&time=1729298905): failed to open stream: no suitable wrapper could be found in /data/40/5/71/99/5397425/user/6768456/htdocs/portal/wp-content/plugins/xt-visitor-counter/xt-visitor-counter.php on line 48