Friday, October 18

Kitaifa

Meneja kampeni Mkoa kusini Pemba awanadi wagombea wa CCM wa jimbo la Ole.
Kitaifa, Siasa

Meneja kampeni Mkoa kusini Pemba awanadi wagombea wa CCM wa jimbo la Ole.

MENEJA kamopeni za Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kusini Pemba, Mohamed Aboud Mohamed amewataka wananchi wa jimbo la Ole Wilaya ya Chake Chake, kuitumia bahati ya kipekee ya kupata viongozi wenyenia ya kuwatumikia wananchi wajimbo hilo Alisema jimbo la ole katika miaka mingi iliyopita, lilikuwa chini ya utawala wa chama cha CUF, huku wananchi wakikosa maendeleo waliokuwa wakiahidiwa na viongozi walioowachagua. Meneja huyo aliyaeleza hayo wakati alipokuwa akiwanadi wagombea ubunge, uwakilishi na udiwani wa jimbo hilo, katika mkutano wa hadhara wa kampeni zilizofanyika unja wa mpira Vumba Vitongoji. Alisema wananchi wa jimbo la Ole wanakila sababu kuwachagua wagombea wa wote wa CCM, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ili viongozi hao waweze kuwatumikia. “Kazi yenu ni kwenda k...
Rais wa UTPC atua PPC.
Kitaifa

Rais wa UTPC atua PPC.

Viongozi wa Vilabu vya waandishi wa habari nchini wametakiwa  kuwa na mashirikiano ya kutosha na wanachama wa vilabu hivyo ili waweze kutumikia wananchi  kwa ufanisi zaidi. Wito huo umetolewa na Rais wa  Umoja wa Vilabu vya waandishi wa habari Tanzinia   (UTPC ) Deogratias  Nsokolo wakati alipokuwa akizungumza na uongozi wa Klabu ya Waandishi wa habari Kisiwani Pemba ( Pemba Press Club)  huko ofisini kwao Misufini Chake Chake  Pemba . Amesema waandishi wa habari   wanajukumu la kusaidia kupaza sauti za wasio na sauti ili waweze kusikika  na kuchukuliwa hatua kwa changamoto zao zinazowakabili hivyo bila ya kuwepo mashirikiano ya dhati kazi hio haiwezi kufanyika ipasavyo. Amesema wananchi hasa wa vijijini wamekabiliwa  na changamoto nyingi hivyo waandishi wa habri ndio wenye...
WAFANYAKAZI wa Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Pemba, wametakiwa kuendelea kulinda nidhamu na heshima ya kazi.
Kitaifa, Sheria

WAFANYAKAZI wa Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Pemba, wametakiwa kuendelea kulinda nidhamu na heshima ya kazi.

  RAIYE MKUBWA – WVUSM.   WAFANYAKAZI wa Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Pemba, wametakiwa kuendelea kulinda nidhamu na heshima ya kazi kwa kutozungumzia siasa wakiwa sehemu ya kazi, pamoja na kuacha kujiingiza katika makundi ambayo mwisho wake yatapelekea kuingia matatizoni wakati huu wa kuelekea Uchaguzi. Hayo yameelezwa na Afisa Mdhamini Wizara ya Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Fatma Hamad Rajab, alipokua akizungumza na Wafanyakazi wa Wizara hiyo katika Ukumbi wa Mkutano wa Wizara ya Fedha na Mipango Gombani Wilaya ya Chake Chake. Alisema baada ya uchaguzi serikali inaendelea, aliwataka kuendelea kulinda heshima nidhamu ya kazi panoja na kutokujiingiza katika mambo yasiowahusu. Aidha, amewasisitiza wafanyakazi hao kutokubali kutumiwa vibaya...
CHADEMA wafungua kampeni Mtambile.
Kitaifa, Siasa

CHADEMA wafungua kampeni Mtambile.

  MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha Demokrasia Maendeleo Chadema Said Issa Mohamed, amesema iwapo wananchi wa Zanzibar wampatia ridhaa ya kuongoza nchi, atahakikisha anatumia rasilimali ziazopatikana nchini kwa kuipaisha Zanzibar kiuchumi. Alisema atatumia rasilimali hizo kwa kuunda viwanda mbali mbali ambavyo, vitaweza kuifanya Zanzibar kuzalisha bidhaa ikiwemo mboga mbona na kuuza katika masoko makubwa ulimwenguni. Mgombea huyo aliyaeleza hayo huko kangani Wilaya ya Mkoani, wakati wa ufunguzi wa kampeni za jimbo la Mtambile na kuwanadi wagombea ubunge na uwakilishi wa jimbo hilo. Alifahamisha kuwa watahakikisha wanaelimisha vijana kujikita katika kilimo, kwani Zanzibar inauwezo wakuzalisha kwa wingi mchele na kuuzwa kilo shilingi 300. Alisema iwapo ata...
Umasikini ni chanzo za udhalilishaji.
Kitaifa, Siasa, Wanawake & Watoto

Umasikini ni chanzo za udhalilishaji.

UMASKINI uliokithiri  imebainika kuwa  ni moja ya  sababu inayopelekea  Watoto   kufanyiwa  Udhalilishaji. Hayo yamesemwa na wdau wa mtandao wa kupinga udhalilishaji kutoka Wilaya ya Mkoani, katika mkutano wa uwasilishaji wa ripoti za utekelezaji wa majukumu yao ya kutoa elimu  juu ya madhara ya udhalilishaji wa kijinsia kwa jamii uliofanyika ofisi ya TAMWA Pemba. Kwa upande wake Shaban Juma Kassim Msaidizi wa sheria kutoka  shehia ya Mkanyageni, alifahamisha  kuwa udhalilishaji unafanyika zaid kwa watoto  wanaokosa  malezi  ya  pamoja  ambao wazazi wao wameachana. Alisema  takriban  watoto  wengi ambao wazazi wao wameachana, wanakosa masomo na badayake wanatumikishwa ili wapate mahitaji yao  hali ambayo inaridisha nyuma maendele ya watoto. ‘’Wanawake wengi hususan wanaois...