Friday, October 18

Kitaifa

Mahakama yamrejesha uraiani aliyedaiwa kumuingilia mlemavu Pujini
Kitaifa, Sheria, Wanawake & Watoto

Mahakama yamrejesha uraiani aliyedaiwa kumuingilia mlemavu Pujini

IMEANDIKWA NA HAJI NASSOR, PEMBA MAHAKAMA ya mkoa Chake Chake, imemuachia huru, kijana Abdalla Khatib Abdalla miaka 25 wa Pujini, aliyekuwa akituhumiwa kumuingilia mwanamke mwenye ulemavu wa akili, baada ya mahakama hiyo kubaini utata juu ya eneo alililodaiwa kuingiliwa mwanamke huyo. Hakimu wa mahakama hiyo Luciano Makoye Nyengo, alisema kuwa, amelazimika kumuachia huru mtuhumiwa kwa vile, shahidi mmoja alidai mwanamke huyo aliingiliwa kichani tena chini ya Muwembe. Alisema, ilipofika wakati wa shahidi muathirika ambae ana ulemavu wa akili, aliimbia mahakama hiyo kuwa, aliingiliwa na mtuhumiwa ndani ya nyumba eneo la Pujini na sio kichakani. “Shahidi mmoja alidai kuwa, tukio la kuingiliwa kwa mwanamke huyo lilifanyika kichakani, ingawa alipokuja muathirika wa tukio, aliiel...