Saturday, March 15
WAZIRI wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar afungua Ofisi ya Elimu na Mafunzo ya Amali Wilaya ya Wete .
ELIMU

WAZIRI wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar afungua Ofisi ya Elimu na Mafunzo ya Amali Wilaya ya Wete .

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA WAZIRI wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Simai Mohamed Said, amesema wananchi wa Zanzibar wanakila sababu ya kuyalinda, kuyaenzi na kuyadumisha Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964, kwani yamepelekea wazanzibar kuwa wamoja na kufanya shuhuli zao kwa amani na utulivu. Alisema hivi sasa Zanzibar ipo katika serikali ya Umoja wa kitaifa hakuna ubaguzi wa kisiasa, huku akiwapongeza walimu kwa kuendelea kutoa elimu bora kwa wanafunzi wao, bila ya kujali siasa zao kwani muda wake haujafika. Waziri Simai aliyaeleza hayo wakati alipokua akizungumza na walimu, wananchi wa Wilaya ya Wete mara baada ya ufunguzi wa Ofisi ya Elimu na Mafunzo ya Amali Wilaya ya Wete, Mitiulaya ikiwa ni shamrashamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar. Aidha alisema Serikali ya awamu ya nane ...
Bonanza la Michezo kwa taasisi za Serekali lazinduliwa kisiwani Pemba.
Kitaifa, Michezo

Bonanza la Michezo kwa taasisi za Serekali lazinduliwa kisiwani Pemba.

YOTE HII NI KASI YA DR. MWINYI ,BONANZA LA MICHEZO LINAWEZEKANA. Na Maryam Taalib - -Pemba. MKUU wa Wilaya ya Chake Chake  Abdalla Rashid  amewataka watendaji wa Taasisi pamoja na wananchi kwa ujumla kujenga utamaduni wa  kuimarisha afya zao kupitia michezo tofauti  ili kuondokana na kupata maradhi hatarishi. Ameyasema hayo wakati akizindua Bonanza  la michezo  katika uwanja wa Gombani Kongwe Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba ikiwa ni katika heka  heka za kusherehekea kwa kutimiza miaka (60) ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Alisema  amefarajika kwa kiasi kikubwa kuona wanataasisi wamejitokeza kwa wingi katika mashindo hayo ya michezo tofauti tofauti. Hata hivyo Mkuu wa Wilaya alimpongeza  Ofisa  Mdhamini Wizra ya Habari Vijana Utamaduni  na Michezo Pemba M...
Wizara ya Habari yazindua shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa kufanya usafi Wilaya ya Mkoani.
afya

Wizara ya Habari yazindua shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa kufanya usafi Wilaya ya Mkoani.

Na Maryam Talib – Pemba Ofisa Mdhamin Wizara Habari Utamaduni na Michezo Mfamau Lali Mfamau katika kuelekea kuadhimisha miaka (60) ya Mapinduzi  Matukufu ya Zanzibar aliwataka wananchi wa maeneo tofauti kujenga Utamaduni wa kusafisha katika maeneo yao yaliyowazunguka kwa lengo la kuepusha kujitokeza kwa maradhi hususani ya miripuko ikiwemo kipindupindu. Mfamau aliyaeleza hayo alipokuwa akifanya usafi akiwa na watendaji wenzake wa Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Pemba pamoja na wanachi wa Wilaya ya Mkoani huko wilayani kwao. Alisema kuwa ijengwe tabia hiyo ya kufanya usafi na sio kusubiri kila kipindi Fulani au Serikali itangaze tarehe ya kufanya usafi wananchi wenye wanapaswa kujenga utamaduni huo kwa kujipangia muda wa kulitekeleza zoezi hilo. “Nawaombeni...
Jumla ya Miradi 23 kusini Pemba  inatarajiwa kufikiwa kuelekea kilele cha Sherehe za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar.
Kitaifa

Jumla ya Miradi 23 kusini Pemba inatarajiwa kufikiwa kuelekea kilele cha Sherehe za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar.

Na Thureya Ghalib ,Pemba. Jumla ya Miradi 23 inatarajiwa kufunguliwa kuzinduiwa pamoja  na kuekewa mawe ya msingi katika Mkoa wa Kusini Pemba ikiwa ni shamra shamra za kuekelea kilele cha Sherehe za miaka 60 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar . Hayo yamelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Masoud alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari huko ofisini kwake Wilaya ya Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Mattar amesema miradi 10 itafunguliwa katika Mkoa huo ,miradi 4 itazinduliwa na miradi  9 itaekewa mawe ya msingi ,ambayo inahusu masuala ya maendeleo ya Wananchi . Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka Wananchi kushirikiana katika shughuli zote ,kwani sherehe hizo hasihusiani na masuala ya kisiasa au itikadi zozote. Pamoja na hayo ametoa Wito kwa Wananchi kushiriki kat...