NA ABDI SULEIMAN, PEMBA
WAZIRI wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Simai Mohamed Said, amesema wananchi wa Zanzibar wanakila sababu ya kuyalinda, kuyaenzi na kuyadumisha Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964, kwani yamepelekea wazanzibar kuwa wamoja na kufanya shuhuli zao kwa amani na utulivu.
Alisema hivi sasa Zanzibar ipo katika serikali ya Umoja wa kitaifa hakuna ubaguzi wa kisiasa, huku akiwapongeza walimu kwa kuendelea kutoa elimu bora kwa wanafunzi wao, bila ya kujali siasa zao kwani muda wake haujafika.
Waziri Simai aliyaeleza hayo wakati alipokua akizungumza na walimu, wananchi wa Wilaya ya Wete mara baada ya ufunguzi wa Ofisi ya Elimu na Mafunzo ya Amali Wilaya ya Wete, Mitiulaya ikiwa ni shamrashamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar.
Aidha alisema Serikali ya awamu ya nane ...