Saturday, March 15
Vijana wametakiwa kutambua vyema kinachoendelea katika masuala kusimamisha Utawalaa bora 
vijana

Vijana wametakiwa kutambua vyema kinachoendelea katika masuala kusimamisha Utawalaa bora 

    Na Maryam Talib – Pemba.  Ofisa Mdhamin Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora Pemba Halima Khamis Ali aliwataka vijana kutambua vyema kinachoendelea katika masuala kusimamisha Utawalaa bora  katika maeneo tofauti  kwani vijana ndio nguvu kazi ya taifa kusudi kuwa mabalozi wazuri katika jamii zetu. Aliyasema hayo alipokuwa akifungua mkutano wa siku moja uliowashirikisha vijana 40 kutoka shehia tofauti za Wilaya Chake Chake uliofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala bora kisiwani Pemba. Mdhamin  huyo alisema mafunzo hayo ya Rshwa na utawala bora ,ajira  yamefanyika kwa vijana kwani wao ndio wahusika katika maswala  mengi vijana kwani taifa imara ni taifa lenye vijana wengi lakini  wawe na uzalendo  na uchun...
Vijana kisiwani Pemba wametakiwa  kuuchangia vyema Mpango mkakati wa kitaifa.
vijana

Vijana kisiwani Pemba wametakiwa kuuchangia vyema Mpango mkakati wa kitaifa.

Na Maryam Talib – Pemba. Ofisa Mdhamin Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo  Pemba Mfamau Lali Mfamau amewataka baadhi ya vijana kisiwani Pemba kuibua na kuuchangia vyema Mpango mkakati wa kitaifa katika vipengele vyote ambavyo vimeainishwa katika mpango huo utakaowasilishwa na washauri elekezi wa mpango huo. Aliyasema hayo alipokuwa akifungua mafunzo yaliyoendeshwa kwa siku mbili yaliyowashirikisha vijana wenye mahitaji maalumu , vijana wa mitaani , vijana walio sober house, na kundi la wanasiasa kutoka maeneo tofauti ya kisiwa cha Pemba  katika ukumbi wa Wizara ya fedha  na ukumbi wa Makonyo Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba. Mdhamini huyo aliwaambia vijana hao hiyo ni fursa ya kipekee ambayo wamepatiwa hivyo kutoa michango iliyo bora ili iweze kuleta m...
Wamiliki wa vyombo vya habari wametakiwa kujisajili Tume ya Utangazaji.
Sheria

Wamiliki wa vyombo vya habari wametakiwa kujisajili Tume ya Utangazaji.

  Na Maryam Talib – Pemba.  Ofisa Mdhamin Wizara ya habari Vijana Utamaduni na Michezo Mfamau Lali Mfamau amewataka wamiliki wa vyombo vya habari hususani  online tv wasajili vyombo vyao  Tume ya utangazaji kwa lengo la kuondosha shubha ama changamoto  zinazojitokeza katika kazi zao. Aliyasema hayo alipokuwa akifungua mapitio ya sheria ya tume utangazaji yaliyofanyika katika ukumbi wa uwezeshaji Gombani Kisiwani Pemba Mdhamini huyo alisema lengo la kufanya hivyo ni kuona vyombo vyote vinatoa taarifa zake kwa jamii iwe zinaendana na mazingira ya watu na endapo itatokezea  tatizo kwenye taarifa iwe ni wepesi kuelekezana na kurudi kwenye mstari kwani kila binadamu ana mapungufu yake. “Na nyinyi watu wa tume nawambia iwe basi mana kuna watu wengine wanadharau kuvunja ut...
ZRA imezindua kampeni ya Home Stay.
Biashara

ZRA imezindua kampeni ya Home Stay.

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA MAMLAKA ya Mapato Zanzibar (ZRA) imezindua kampeni ya Home Stay, yenye lengo la kutambua majengo ambayo hayajasajiliwa na yanalaza wageni ndani ya Wilaya ya Chake Chake. Hayo yameelezwa na Meneja wa Kodi Pemba kutoka ZRA Ali Khatib, wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo ndani ya Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema kumekua na nyumba nyingi zinalaza wageni ndani ya wilaya hiyo, lakini bado hazijatambulika rasmi na ZRA jambo ambalo linaleta ukakasi. “Kampeni hii leo tuemizindua ikiwa tumo katika mwezi wa shukurani kwa mlipa kodi, na majumba yapo yanayolala wageni ila hayajatambuliwa leo tumeamua kuwapatia elimu wamiliki ili kuweza kuzisajili nyumba zao,”alisema. Alisema kuna umuhimu mkubwa ni kuzitambua na kupeana taaluma, juu ya kuz...
Zaidi ya wakulima 3000 wanapokea fedha zao kupitia TigoPesa
Biashara

Zaidi ya wakulima 3000 wanapokea fedha zao kupitia TigoPesa

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA WAKULIMA wa Zao la karafuu Kisiwani Pemba, wameshauriwa kuendelea kupokea fedha zao kwa kutumia TigoPesa, kufanya hivyo ni kuwasaidia vijana waliojiajiri wenyewe kuwa mawakala wa mitandano ya siku. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa TigoZantel Zanzibar Azizi Said Ali, wakati alipokua akizungumza katika hafla ya chakula cha mchana na utoaji wa zawadi, kwa wakulima wa zao la karafuu Kisiwani Pemba, hafla iliyofanyika Mjini Chake Chake. Alisema wameamua kuwa karibu zaidi na wale wanaoshirikiana nao kwa kukubali kulipwa kutumia TigoPesa, kwani waliokubali kulipwa ni ndugu zao na wametoa sadaka kubwa kwa vijana waliojiajiri kupitia uwakala. Alisema tokea mwaka huu kuanza msimu, zaidi ya wakulima 3439 wamelipwa fedha zao kupitia miamala ya TigoPesa, na kuw...