Video: RC Kusini Pemba “Acheni kujichukulia sheria mikononi”.
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba ambae pia ni Mwenyeiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mkoa Mh. HEMED SLEIMAN ABDALLA amewataka wananchi kuacha tabia ya kuchukuwa sheria mikononi mwao kwani vitendo hivyo vinaweza kuhatarisha uvunjifu wa amanii nchini.
Mkuu wa Mkoa huyo ametowa wito huo huko ofisini kwake Chake Chake wakati akizungumza na ZBC kufuatia tukio la kijana mmoja kuwapinga mapanga watu watatu huko katika kijiji cha Kangagani Wete.
Amesema katika kipindi hichi cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu kumekuwa na mikusanyiko ya watu mbali mbali hivyo kwa wale ambao watahudhuria katika kampeni hizo hawana budi kuhakikisha wanaendelea kudumisha amani na utulivu kwa usalama wao na taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake kamanda wa polisi Mkoa wa Kusini Pemba Msaidizi kamis...