Friday, March 14
VIDEO: Wagombea jimbo la Kiwani wanadi sera zao.
Kitaifa, Siasa

VIDEO: Wagombea jimbo la Kiwani wanadi sera zao.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kiwani  katika Wilaya ya Mkoani ndugu Rashid Abdalla Rashid  amewataka wananchi wa Jimbo hilo kumchagua na kuendelea kukipigia kura Chama cha Mapinduzi  ili kiweze kuwaletea maendeleo wazanzibar na Watanzania kwa ujumla. Ndugu Rashid ameyasema hayo huko Mwambe wakati wa uzinduzi wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi katika jimbo la Kiwani. Amesema katika uongozi wa awamu ya saba inayomalizia kuna miradi mingi ya maendeleo imeekezwa kwa ajili ya kuwaondoshea kero wananchi hivyo ni vyema kuendelea kukiweka madarakani chama cha mapinduzi ili wananchi wazidi kunufaika na maendeleo hayo. Naye mgombea  wa uwakilishi wa jimbo la Kiwani ndugu Mussa Foum Mussa amesema katika kipindi kilichopita wakati akiwa mwakilishi wa jimbo hilo alifanikiwa kusimamia upatiukan...
Waziri Aboud: Waandishi  kuwahamasisha wananchi kutunza  amani ya nchi kuelekea uchaguzi mkuu.
Kitaifa, Siasa

Waziri Aboud: Waandishi kuwahamasisha wananchi kutunza amani ya nchi kuelekea uchaguzi mkuu.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed, amewataka wananchi wa Zanzibar kutokukubali kuchokozeka badala yake kuendelea kudumisha amani ya nchi. Alisema dhamira ya Serikali ni kuendelea kuwaelimisha wananchi, juu ya suala zima la kufahamu umuhimu wa amani katika nchi kabla na baada ya uchaguzi. Waziri Aboud aliyaeleza hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Kisiwani Pemba, juu ya kuwahamasisha wananchi utunzaji wa amani ya nchi kuelekea uchaguzi mkuu wa Zanzibar Oktoba 2020. Alisema ni wakati muhimu sasa kwa wanasiasa kukubali kufanya uchaguzi mkuu kwa salama na amani, pamoja na kuwa walinzi wan chi katika kipindi hiki. “Sisi ni walinzi wa nchi yetu, kumeanza kutokeza dalili ambazo sio nzuri, wananchi serikali imejipanga kuhakiki...
Wanahabari watakiwa kuandika taarifa zinazohusiana na hifadhi , utalii na mazingira.
Biashara, Kitaifa, Makala

Wanahabari watakiwa kuandika taarifa zinazohusiana na hifadhi , utalii na mazingira.

TAKRIBAN hekta Milioni 12 ya misitu katika eneo la Kitropiki ya Dunia limepotea kwa moto mwaka 2018, naweza kusema sawa na kupotea viwanja 30 vya mpira wa miguu kwa dakika. Kwa mujibu wa Ripoti ya Global Forest watch ikionyesha kupungua kwa misitu mwaka 2016 na 2017, licha ya upoteaji huo ulianza tokea mwaka 2001. Kama tunavyojua miti katika eneo hili ni muhimu kwa makaazi ya watu, kutoka makabila mbali mbali ya utoaji wa chakula, miti katika eneo hili muhimu duniani katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.   Mamilioni ya hekta za misitu imekuwa ikipotea katika karne za hivi karibuni, kutokana na shughuli za kibiashara na kilimo, Takwimu za mwaka 2018 zinaonyesha kuna utofauti katika upungufu mkubwa wa misitu kwa miaka miwili iliyopita, miti mingi imepote...
CUF yazindua kampeni Pemba.
Kitaifa, Siasa

CUF yazindua kampeni Pemba.

MGOMBE Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha wananchi CUF, Profesa Ibrahim Haruna Lipumba amesema kuwa CUF inaomba kura kwa sababu chama hicho katika vyama vyote ndicho kinachosimamia haki sawa kwa wananchi wote. Alisema katika jambo ambalo CUF walifanikiwa kulipata Zanzibar katika mapambano ya kisiasa, ni katiba inayozungumzia uwepo wa Serikali ya Umoja wa kitaifa. Profesa aliyaeleza hayo wakati wa ufunguzi wa Kampeni za chama hicho, zilizofanyika katika uwanja wa michezo Tibirinzi mjini Chake Chake Pemba, huku zikihudhuriwa na wanachama na wananchi wa chama hicho. Alisema CUF imekuwa ni waasisi wamaridhiano, waasisi wa mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ambayo imepelekea kuwepo kwa serikali ya umoja wa Kitaifa. “Ndugu zangu nyote mnakumbuka tuliingia ka...
DK. Shein aweka jiwe la msingi Pemba.
Biashara, Kitaifa

DK. Shein aweka jiwe la msingi Pemba.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, amesema kuwa sula la viwanda kwa Zanzibar ni suala la miaka mingi sana, kabla ya Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964 na baada ya Mapinduzi, ikiwemo viwanda vidogo vidogo, vya kati na vikubwa. Alisema viwanda hivyo vilikuwa vya sabuni, usumba, mafuta ya nazi, viwanda vya soda, maziwa, Mapinduzi ya mwaka 1964 ndio yaliobadili maendeleo hayo. Dk.Shein aliyaeleza hayo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Mikoa miwili ya Pemba, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa kiwanda cha kusarifia Mwani uliokwenda sambamba na Uzinduzi wa eneo la Viwanda Chamanangwe II Mkoa wa Kaskazini Pemba. “Zanzibar ilikuwa imenawiri kwa viwanda vidogo vidogo, ikiwemo viwanda vya maziwa, mterekta, soda, kiwanda c...