NA ABDI SULEIMAN, PEMBA.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi, amesema mara baada ya kushika hatamu, tarehe 23 Septemba 1964, Serikali ya Mapinduzi ya awamu ya kwanza iliyoongozwa na Hayati Mzee Abeid Amani Karume, ilitangaza elimu bure, ili kutoa fursa sawa kwa wananchi wake wote kupata elimu bila ya ubaguzi wowote.
Alisema fursa za elimu zilifunguka na kupata elimu ikawa ni haki ya msingi kwa kila raia, hali iliyopelekea Serikali kuweka mikakati mbali mbali katika utekelezaji wa tamko hilo la elimu bure.
Rais Dkt.Hussein Ali Mwinyi aliyaeleza hayo, huko katika viwanja vya skuli ya Sekondari Utaani mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi skuli hiyo, ikiwa ni shamra shmra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Aidha alisema gharama z...