Saturday, March 15
Kilio cha upatikanaji wa maji safi na salama bweni la skuli ya Madungu Sekondari chamaliza.
afya, ELIMU

Kilio cha upatikanaji wa maji safi na salama bweni la skuli ya Madungu Sekondari chamaliza.

  NA AMINA AHMED-PEMBA. KWA zaidi ya Miezi mitatu na siku kadhaa sasa hofu ya usalama wa afya kwa baadhi ya wanafunzi wanaokaa katika bweni Skuli ya Madungu sekondari imeondoka hii ni baada ya kupatikana huduma ya maji safi na salama muda wote skulini hapo, sambamba na kuwepo kwa utaratibu maalum wa uzolewaji wa taka katia eneo wanalotumia kutupa taka mbali mbali. Wakizungumza na habari hizi baadhi ya wanafunzi wanaokaa katika bweni skulini hapo wamesema  kuwa hali ya kuishi kwa wasi wasi na hofu ya maradhi kwa sasa imeondoka hali ambayo imesaidia kuzidisha umakini zaidi katika masomo yao. Aidha wamemshukuru mwandishi wa habari hizi kwa jitihada aliyochukua katika kuhakikisha suala hili linakuwa sawa na kupatiwa ufumbuzi. "Nilipoona maji yanatoka siku iyo hayajafungwa...
Waziri  Mkuya aweka  jiwe la Msingi bustani ya wananchi Mwanamashungi Chake Chake.
Biashara

Waziri Mkuya aweka  jiwe la Msingi bustani ya wananchi Mwanamashungi Chake Chake.

NA AMINA AHMED - PEMBA. WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais fedha na mipango Zanzibar Dk Saada Mkuya Salum amewataka wananchi kutoka maeneo mbali mbali kisiwani Pemba kuitumia bustani ya wananchi inayojengwa na serikali kwa malengo yaliokusudiwa mara itakapokamilika. Ameyasema hayo  alipokuwa akizungumza na wananchi katika sherehe ya uwekeaji jiwe la Msingi bustani ya wananchi Mwanamashungi Chake Chake ikiwa ni muendelezo wa Shamra shamra kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar . Amesema ili malengo ya kujengwa eneo la bustani hiyo ambayo inayotarajiwa kukamilika rasmi mwezi February mwaka huu yaweze kutimia ni vyema wananchi kuitumia katika shughuli mbali mbali ikiwemo uzalishaji wa biashara mbali mbali ambazo zitasaidia kukuza vyanzo vya mapato yatakayotumika kwa shughuli za u...
Waziri Shamata azindua ofisi ya elimu Wilaya ya Mkoani.
ELIMU

Waziri Shamata azindua ofisi ya elimu Wilaya ya Mkoani.

NA AMINA AHMED-PEMBA. Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964 yalilenga kuondosha utawala wa kidhalimu na kuwafanya wananchi kufurahia matunda ya Uhuru kwa kuwaletea maendeleo. Hayo yameelezwa na Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Mifugo na Maliasili Mh. Shamata Shaame Khamis katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Elimu Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba ikiwa ni Miongoni mwa Shamra shamra za maadhimisho ya kutimia miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Amesema katika kupiga hatua kimaendeleo suala la elimu ni muhimu hivyo Serikali imekua ikiimarisha Miundo mbinu ya kielimu ili kusukuma mbele kasi ya maendeleo nchini. Amesema kutokana na jitihada za Serikali za kutatua changamoto za kielimu mafanikio yanaonekana ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa ufaulu katika ngazi mbali m...
Rais Dkt Mwinyi aweka Jiwe la Msingi skuli ya sekondari Maziwang’ombe Wilaya ya Micheweni.
ELIMU

Rais Dkt Mwinyi aweka Jiwe la Msingi skuli ya sekondari Maziwang’ombe Wilaya ya Micheweni.

NA ABDI SULEIMAN, PEMBA RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi, amsema Serikali imeanza utekelezaji wa mageuzi katika mfumo wa elimu, ili kuhakikisha vijana wanapata elimu inayowezesha kukabiliana na changamoto za mazingira yao halisi. Rais Mwinyi aliyaeleza hayo katika viwanja vya skuli ya sekondari Maziwang’ombe Wilaya ya Micheweni, mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi skuli hiyo ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Alisema kuanzia mwaka 2024, Serikali itaanza majaribio ya mtaala mpya wa elimu ya sekondari, mtaala ambao utalenga kujenga ujuzi wa vijana katika fani mbalimbali kwa kuzingatia mazingira yao. “Kwa Maziwang'ombe, hii inamaanisha vijana watapata ujuzi unaoendana na mazingira yaliotuzunguka, ikiwa...